TANGAZA NASI

header ads

Mahakama yaifuta kesi ya kina Halima Mdee na wenzake

 


MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, imewaachia huru viongozi na wafuasi 27 wa Chadema waliokuwa wanadaiwa kufanya mkusanyiko na kuvunja geti la gereza la Segerea chini ya kifungu cha 225(5) cha sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai (CPA.)

Kesi hiyo imefutwa leo Mei 5, 2021 na Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi baada ya upande wa mashtaka kushindwa kupeleka mashahidi mahakamani.

Mapema leo asubuhi kesi hiyo iliitwa kwa ajili ya kuendelea kusikilizwa lakini upande wa mashtaka ukiongozwa na Wakili wa Serikali Mwandamizi  Mkunde Mshanga akisaidiana na wakili wa serikali Ester Martin kudai mahakamani  hapo kuwa kuwa kwa leo hawana shaidi hivyo wameiomba mahakama kuipangia kesi hiyo tarehe nyingine ya kusikilizwa.

Post a Comment

0 Comments