TANGAZA NASI

header ads

Ujumbe wa India katika mkutano wa G7 London wapatikana na Corona

 



Ujumbe wa India unaohudhuria mkutano wa G7 jijini London wamepatikana na virusi ya Corona.

Waziri wa Mambo ya nje wa India Subramanyan Jaishankar Katika mtandao wa twitter amethibitisha kwamba Wajumbe hao sasa wamejitenga na watahudhuria mkutano huo kupitia mtandao.

Afisa wa serikali ya Uingereza alisema washiriki wawili walipimwa na kupatikana na Corona baada ya kufanyiwa uchunguzi wa kila siku katika mkutano huo.

Mkutano huo wa mataifa ya G-7 unaingia siku yake ya mwisho huku mawaziri wa Mambo ya nje wa mataifa hayo wakijadili usambazaji wa chanjo ya corona ulimwenguni.

Shirika la Afya Duniani WHO lilikuwa limehimiza mataifa yalioendelea kusaidia nchi masikini kupata chanjo hizo.

Post a Comment

0 Comments