TANGAZA NASI

header ads

Shule za msingi 24 wilayani Ludewa zapanda kiwango cha ufaulu

 



Na Prosper Mfugale,Ludewa

Asilimia za Ufaulu mitihani ya darasa la saba na la nne katika shule za msingi 24 kutoka kata 6 wilayani ludewa mkoani Njombe zimeanza kupanda Katika maeneo  kunakotekelezwa mradi wa MAMMIE kupitia shirika la maendeleo kusini mwa Tanzania SHIPO kwa ufadhili wa  shirika la kimataifa la we world ambapo shule ya msingi mavala kutoka kata ya milo imefanikiwa kuchomoza na kuongoza katika mtihani wa darasa la saba kwa shule zote za serikali wilayani humo.

Shule hizo zipo katika kata za milo, lubonde,mlangali,madope,mawengi,na luana ambazo zimejengewa miundombinu ya majengo yakiwemo madarasa, ofisi ,majiko ,mabwalo ya chakula, matundu ya vyoo na miundombinu ya maji

Shirika la Shipo katika taarifa yake kupitia mratibu wa mradi wa MAMMIE bwana nemes temba kwenye kilele cha  madhimisho ya wiki ya elimu duniani yaliyofanyika katika shule ya msingi mavala hapo may 5, 2021 alieleza kuwa  juma la elimu duniani hufanyika kila mwaka ifikapo  apri 26-30 lakini mwaka huu siku maadhimisho yamesogea mbele kutokana na kuingiliana na ratiba za mitihani za wilaya ya ludewa

Aliongeza kuwa kauli mbiu ya juma la elimu kwa mwaka 2021 ni wezesha elimu stawisha jamii ambapo alisema siku hiyo ipo katika ajenda 17 zaa maendeleo endelevu  kwenye lengo namba nne linalosisitiza kutoa elimu ya usawa, elimu jumuishi  

Tangu mwaka 2014 shirika la shipo baada ya kutambua kuwa changamoto mbalimbali zilizopo katika shule za msingi hurudisha nyuma jitihada za kupandisha ufaulu lilianza kubresha miundombinu katika shule hizo kwa kusaidia ujenzi wa mindombinu kwa awamu ambapo mpaka sasa lipo katika awamu ya tatu ndani ya kata hizo sita .

Licha ya kusaidia katika mradi  huo shirika pia lilitoa mafunzo kwa walimu wazazi na kamati za shule yanayohusu utawala bora ili kuwa na uelewa mpana juu ya masuala yahusuyo elimu.

‘’hasa tuanasaidia katika kuboresha utawala na usimamizi ,tunaboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia kama mujenzi wa vyoo madarasa ,nyumba za walimu majiko na mabwalo ya chakula lakini pia tunasaidia kuweka miundombinmu ya maji shuleni’’Nemesi temba mratibu mradi wa mammie Shipo Njombe.

Shirika la Shipo pia lilitoa msaada wa miche ya miti ya mbao na matunda ina ya parachichi katika shule za msingi 24 wilayani ludewa kutoka kata 6 ili kusaidia kujiwezesha kiuchumi wakati wa kipindi cha mavuno.

‘’Kwa kata ya milo tulipokea miche 510 ya matunda ambayo kwa sasa ina umri wa mika 3 na inatoa matunda na Watoto wanapata chakula cha mchana huku wakifurahia mlo wenye matunda na mboga za majani. Alisema sijali simindu afisa ogani kata ya milo

Kila mwaka shirika huadhimisha  wiki ya elimu duniani ambapo siku hiyo shule iliyofanya vizuri hupewa zawadi mbalimbali ikiwemo kombe la elimu Pamoja na shughuli mbalimbali ambazo hufanyika kwa lengo la kuhamasisha wazazi kuona umhimu wa elimu kwa Watoto wao na kuongeza ari ya masomo kwa wanafunzi kwa kuwapa zawadi mbalimbali vikiwemo vifaa vya vya shule .

Mwaka huu 2021 kilele cha wiki ya elimu kimefanyika katika katika shule ya msingi mavala kata ya milo shule ambayo pia ilifanya vizuri katika mtihani wa darasa la saba mwaka 2020 na kuibuka mshindi kwa shule zilizopo katika mradi kwa kuwa nafasi ya kwanza ambayo ilijinyakulia zawadi mbalimbali likiwemo kombe la elimu.

Shule hii pia iliongoza shule za serikali katika mtihani huo wa mwaka 2020 kwa kushika nafasi ya kwaza na kuwa nafasi ya pili kiwilaya baada ya kuongozwa na shule moja ya binafsi ikiwa ni matokeo chanya yaliyotokana na mradi.

Kwa niaba ya wanafunzi wote wa shule ya msingi mavala mwanafunzi judithi haule alitoa shukrani kwa shule hiyo kuchaguliwa kuadhisha wiki ya elimu ambaye pia alilishukuru shirika kwa misada mbalimbali linayoitoa ambayo imechangia taaluma kupanda.

Wageni mbalimbali walihudhuria katika siku hii mhimu ya kilele cha wiki ya elimu akiwemo afisa elimu msingi wilaya ya ludewa Daniel makorere ambaye alimwakilisha mkurugenzi ambaye Pamoja na mambo mengine alilishukuru shirika la shipo Pamoja na wafadhili kwa kazi nzuri wanazofanya katika idara ya elimu msingi huku akiwataka wazazi kuendelea kushirikiana nao.

 

Wazazi na walimu kutoka shule ya msingi mavala katika siku ya maadhimisho wameleza namna walivyoshiriki katika kuinua elimu ikiwemo ujenzi wa miundombinu na kushiriki katika mradi wa kilimo cha parachichi ulioanzishwa shuleni hapo na wafadhili wa kutoka shirika la kimataifa la we wold  kupitia shirika la shipo kwenye mradi wake wa mammie

Wa kwanza kulia pichani ni mwalimu mkuu wa shule ya msingi Mavala wilayani Ludewa akikabidhiwa kombe la elimu na afisa elimu msingi kutokana na shule hiyo kushinda kitaalamu kati ya shule zinazofadhiliwa na mradi wa Mammie chini ya shirika la shipo

 

 

 

 

Baadhi ya walimu wakikabidhiwa zawadi kwenye maadhimisho ya wiki ya elimu yalifoanyika katika shule ya msingi Mavala kata ya Milo

 

Baadhi ya walimu na watendaji wa shirika la Shipo wakiwa katika picha ya pamoja

 

 

 

 

 

 

 

Post a Comment

0 Comments