TANGAZA NASI

header ads

Shule zakabiliwa na uhaba wa madawati 1250 mjini Makambako

 



Na Amiri Kilagalila,Njombe

Shule za msingi na sekondari halmashauri ya mji wa Makambako mkoni Njombe zinakabiliwa na uhaba wa madawati 416 kwa shule za msingi na 834 kwa shule za sekondari ikiwemo viti na meza kwaajili ya matumizi ya wanafunzi hali inayopelekea changamoto katika utoaji elimu.

Hayo yamebainishwa katika kikao cha baraza la madiwani na mwenyekiti wa halmashauri hiyo Hanana Mfikwa pamoja na mkurugenzi wa halmashauri ya mji huo Paul Malala.Wamesema sio madawati bali pia kuna uhaba mkubwa wa vyumba vya madarasa ambapo wamewaomba madiwani kuwahasisha wananchi  na wadau wengine kujitokeza  kuchangia.

“Tuhamasishe wananchi kuhakikisha wanachangia na kuondoa hili tatizo la madawati na meza kwa shule za msingi na sekondari”alisema Malala

Naye hanana Mfikwa alisema “Ni kweli watoto wamekuwa wengi na wanahitaji kupata huduma kwa hiyo sambamba na hayo tukahamasishe ujenzi wa madarasa kwasababu miundombinu haitoshi pia”alisema Hanana Mfikwa

Madiwani wa halmashauri hiyo mara baada ya kupokea taarifa ya kushirikisha wazazi na wadau uchangiaji wameshauri serikali kuwe na utaratibu wa uchangiaji vifaa kwa wanafunzi wanaotoka katika shule za   nje ya  kata husika.

“Madawati haya ili tuweze kufanikisha inabidi tufanye kama wilaya nyingine kwasababu unapopoeleka kwenye wilaya nyingine wanasema itabidi utoa mchango wa madawati na huko tunalipa shilingi elfu arobaini”alisema Edo chaula diwani kata ya mwembe togwa

Aidha katika kikao hicho madiwani wameonyesha kusikitishwa na kasi ya ukarabati wa barabara za mijini na vijijini zinazosimamiwa na Tarura kwa kuwa maeneo mengi yamekuwa  na changamoto huku TARURA wakisema zinaendelea kukarabatiwa.

Post a Comment

0 Comments