Na Amiri Kilagalila,Njombe
Ili kukidhi ubora na kuingia katika
masoko ya ushindani,wakulima wa zao Parachichi Nchini Tanzania wametakiwa
kutumia mbolea za asili badala ya kutumia mbolea zenye kemikali hali
inayosababisha anguko la zao hilo sokoni.
Wito huo umetolewa na mkurugenzi
mtendaji wa kampuni ya GUAVAY Ahad Katera
wazalishaji wa mbole mbali mbali ikiwemo Mbolea maalum katika zao la
Parachichi Mbolea za HAKIKA,mara baada
ya kufungua mafunzo rasmi kwa ajili ya wasimamizi wa mashamba ya Parachichi
zaidi ya 70 wanaosimamia zaidi ya ekari 900 za mashamba ya Parachichi mkoani
Njombe.
“Uwekezaji katika zao la parachichi
unafanywa na watu tofauti tofauti,wakulima wa kati na wakubwa lakini ushauri na
elimu wanaoupata katika kusimamia mashamba sio wa kitaalamu”Alisema Katera
Ameongeza kuwa “Kilimo cha parachcichi
mkoani Njombe kinakuwa haraka sana lakini elimu na mafunzo ya ubora ni sehemu
ambayo inatakiwa tuiwekee mkazo.Kampuni ya Guavay inazalisha Mbolea ambazo ni
asili ili kusudi mkulima anayelima Parachichi ambayo ni Organic kuwa na
utofauti wa bei na watu wengine”Aliongeza Katera
Wasimamizi wa mashamba ya Parachichi ambao ni wakulima
mkoani Njombe akiwemo Chesco Mkolwe,Yohanes Njawike na Christina Myonga wamesema
kilimo cha mazoea kimekuwa kikiwaingiza kwenye hasara kubwa na hii inatokana na
kukosekana kwa wataalamu wa kutosha wa kilimo ambao wanaweza kuwapa elimu sahihi
ya matumizi ya mbolea na dawa,hivyo kutokana na elimu iliyotolewa na wataalamu
hao itasidia kuipga hatua kwenye kilimo.
“Sisi tunalima kilimo cha kuigana
wenyewe kwa wenyewe kwa kuwa hatuna wataalamu wa kutuelekeza nah ii inatuathiri
kwa kiasi kikubwa sana huku mashambani,kwa hiyo hapa leo tumejifunza mengi
ambayo pia yanapunguza ghalama ya uzalishaji”alisema Chesco Mkolwe
Musa Makumba na Rebeca Mwepelwa ni
wataalamu wa kilimo kutoka makampuni tofauti hapa nchini ambao wanatumia fursa
hiyo kuwataka wakulima kuzingatia kanuni bora za kilimo na kulima kilimo hai.
“Sisi tunachotaka ni kufikia kwenye
viwango vya kimataifa na kuweza kuhakikisha tunashirikiana kuhakikisha mtu
anayetumia mbolea za kilimo hai atofautishwe na mtu anayetumia mbolea za Chumvi
chumvi”alisema Musa Makumba
Kampuni ya GUAVAY ya jijini Dar Es Salaam ianayozalisha mbolea za Hakika ambazo ni
asili imefika katika maeneo mbali mbali
ya wakulima Nchini nchini huku mkoani Njombe ikifanya kazi na mawakala
ili kuhakiksha inawafikia wakulima vijijini kwa bei naafu.
0 Comments