TANGAZA NASI

header ads

Soko la uuzaji madini lazinduliwa mkoani Njombe




Na Amiri kilagalila,Njombe
Serikali mkoa wa Njombe imezindua soko la uuzaji wa madini ya dhahabu na vito kwa nia ya kudhibiti wimbi la utoroshaji wa madini uliokuwa unafanywa na wachimbaji waliokuwa wakikwepa kulipa mapato ya serikali.
Akizungumza katika  uzinduzi huo uliofanyika katika eneo la ofisi za madini mkoa wa Njombe zilizopo Nazareth kata ya mji mwema halmashauri ya mji wa Njombe,mkuu wa mkoa wa Njombe Christopher Ole Sendeka amesema kuwepo kwa soko hilo la madini itasaidia wachimbaji hao kutumia fursa na njia zilizosahihi kulipa mapato kwa serikali.
“Kuanzisha soko la madini katika mkoa wetu inakuwa ni fursa ya serikali katika kukusanya mapato yake yanayotokana na madini, lakini pia eneo letu hili la soko la madini litakalokuwa pia eneo linalotoa elimu ya uchimbaji wa madini kwa njia ya kisasa na kueleza kuwaunganisha wananchi na wawekezaji wengine wenye nia ya kuwekeza mkoani Njombe"alisema  Ole Sendeka.
Ole Sendeka alisema mkoa wa Njombe unayo rasilimali nyingi ya madini mbalimbali ikiwemo aina tofauti ya vito, hivyo ni vyema wachimbaji wa madini wakaendelea kuhamasisha wawekezaji mbalimbali wakaja mkoani hapa kuwekeza kwa maslahi mapana ya taifa.
“Nampongeza sana Rais Dkt. Magufuli kwa kuhakikisha kwamba rasilimali na  utajiri wa nchi yetu unatumika kwa manufaa na maslahi mapana ya nchi yetu, sasa namna bora ya kumuunga mkono Rais ni kuhakikisha madini yetu yanazalishwa bila kujali madini ya kiwandani madini ya vito yanapitwa katika mfumo na yanauzwa katika utaratibu rasmi uliowekwa na serikali”alisema Ole Sendeka.
Kwa upande wake,kamishina wa madini mkoa wa Njombe, Wilfred Machumu alisema mkoa wa Njombe changamoto iliyopo kwa sasa ni utoroshaji wa madini kwenye baadhi ya maeneo yaliyopo mkoani humo hali inayosababisha kuikosesha mapato serikali.
“Utoroshaji wa madini upo mkubwa sana katika mkoa wa Njombe,hasa maeneo ya Uwemba,Lola Lupembe na Mfumbi Makete, yale maeneo ndiyo yanayotusumbua sana na hayo ndiyo takwimu zinaonyesha kuwa ndiko kwenye utoroshaji mkubwa sana,tumepanga kuongeza nguvu katika kuyafatilia maeneo hayo kuhakikisha hakuna jambo hilo"alisema Machumu.
Baadhi ya wachimbaji wa madini akiwemo Abusalum Sanga walimweleza Ole Sendeka kuwa mkoani Njombe rasilimali ya madini ni nyingi isipokuwa changamoto iliyopo ni kukosekana kwa vifaa vya kusaidia uchimbaji wa madini ya aina mbalimbali kwenye mkoa wa Njombe ikiwemo madini aina ya shaba ambayo walisema iko kwenye ubora wa juu tofauti na maeneo mengine hapa nchini.
“Tatizo linalotukwami sisi wachimbaji hapa Njombe ni kukosekana kwa mashine ambazo zingekuwa mkombozi mkubwa na tungekuwa mbali sana kwenye uchimbaji wa madini hapa mkoani, dhahabu iliyopo kata ya Ibumi ni nzuri na safi lakini kikwazo ni vifaa vya kuchimbia vinatuangusha"alisema Sanga.
Kwa upande wa mwenyekiti chama cha wachimbaji madini mkoa wa Njombe Alfred Luvanda alisema soko hilo litajenga imani ya uwekezaji sekta ya madini kwa wakazi wa mkoa huo kinyume na hapo awali

Post a Comment

0 Comments