Na Mwandishi Wetu Mara.
Kesi ya mauji ya kijana wankuru Nyamhanga mkazi wa Buriba Wilayani Tarime Mkoaii Mara inayomkabili Mfanyabiashara Wilayani Tarime imehairishwa kwa mara nyingine kutokana na upelelezi wake kutokamilika.
Mfanyabiashara huyo anayefaamika kwa jina la Lucas Sotel anatuhumiwa kwa kosa la Mauji ya Kijana Wankuru Nyamuhanga ambayo yalitendeka Agosti 09 mwaka 2014 katika kijiji cha Buriba Wilayani Tarime.
Mwendesha Mshitaka wa jeshi la Polisi Bukombe Bukuru ameiambia Mahakama kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika nakupelekea kesi hiyo kupangwa tena Mnamo June 04 Mwaka huu.
Kwa upande wake Hakimu Mkazi Mahakama ya Wilaya ya Tarime Mh Veronica Mgendi ameharisha kesi hiyo ambapo itatajwa tena Maye Nne Mwaka huu.
Mtuhumiwa amerudishwa Mahabusu mpaka upelelezi utakapokamilika kutokana na mahakama hiyo kutokuwa na uwezo wa kusikiliza kesi inayomkabili Mfanyabishara huyo
0 Comments