TANGAZA NASI

header ads

China yatia nanga barani Afrika.

  Rais wa China amwapisha kiongozi mpya Hong Kong - Mwananchi
China imesema itafuta mikopo isiyokuwa na faida iliyokuwa kama mzigo kwa mataifa mbalimbali ya Afrika wakati huu ambapo nchi za bara la Afrika  linalopoendelea kukabiliana na janga la Corona.

Akizungumza na viongozi wa nchi hizo kupitia mfumo wa Video, rais Jinping pia amezitaka taasisi za fedha za China kuwa na mazungumzo ya kirafiki na nchi za Afrika kuona namna watakavyolipa madeni yao.

Aidha, katika hatua nyingine, amesema nchi yake itasimama na bara la Afrika katika vita dhidi ya Corona na kufadhili ujenzi wa makao makuu ya kudhibiti magonjwa barani Afrika jijini Addis Ababa.

Bara la Afrika kwa sasa lina maambukizi zaidi ya Laki Mbili na vifo zaidi ya Elfu saba kutokana na janga la Corona.

Post a Comment

0 Comments