TANGAZA NASI

header ads

Makambako:Wananchi waendeleza maeneo yaliyozuiwa

Eneo la hifadhi ya Msitu wa Makere... - Wizara Ya Ardhi, Nyumba Na ...

Na Clief Mlelwa,Makambako

Baadhi ya wananchi wa mtaa wa Magongo uliopo kata ya Makambako mkoani Njombe wameamua kuendeleza maeneo yao kwa kujenga nyumba licha ya serikali kuzuia wasiendeleze kwa madai ya kwamba eneo hilo ni la hifadhi ya msitu wa halmashauri.

Wananchi hao wamesema kuwa wameamua kujenga nyumba hizo baada ya kukaa takribani miaka 30 bila kupatiwa suruhisho ya kuendeleza maeneo hayo licha ya kuwa ni maeneo yao halali.

Aidha wananchi hao wamesema kuwa kitendo cha serikali kusema wasiendeleze maeneo hayo kimepelekea wapate adha kubwa hasa kiuchumi.

Nae mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa magongo NICODEM MAKINDA amesema kitendo cha wananchi kuamua kuendeleza maeneo yao ni ishara tosha kwamba wamechoka kusubiri maamuzi ya mwisho kutoka kwenye mamlaka husika hasa serikali.

Hata hivyo mkurugenzi wa halmashauri ya mji wa Makambako PAULO MALALA amesema kuwa hana taarifa ya wananchi hao kuendeleza maeneo hayo na kueleza kuwa endapo yanaendelezwa basi watakuwa wamevamia kwa kuwa eneo hilo halijaruhusiwa kuendelezwa kwa shughuli yoyote.

Post a Comment

0 Comments