TANGAZA NASI

header ads

Wadau 162 wakutana Njombe kujadili namna ya kukabiliana na virusi vya Ukimwi



Na Joctan Myefu,Njombe

Watu wanaopindukia 162 kutoka halmashauri kumi na tano wakiwemo waratibu wa ukimwi  wamekutana mkoani Njombe kujadili namna ya kukabiliana na ugonjwa wa ukimwi kupitia mradi wa hebu tuyajenge  ili  kufikia asilimia tisini na tano tatu hapa nchini.

Mradi huo unaotekelezwa na baraza la taifa la watu wanaoishi na mambukizi ya virusi vya ukimwi Nacopha kwa ufadhili wa serikali ya watu wa Marekani USAID ambapo katika kanda ya Mbeya umefanyika mkoani Njombe ukianza na washiriki kutoka halmashauri tisa.

Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo wakiwemo watu wanaoishi na virusi vya ukimwi akiwemo daud kisunga,john msamvu na joyce samson  wamesema hali ya unanyanyapaa wa watu wanaoishi na maambukizi ya virusi vya ukimwi imepungua kutokana na kuongezeka kwa uelewa kuhusu ukimwi na virusi vya ukimwi huku changamoto ikibaki ndani ya familia. 

Wakizungumzia mradi huo washiriki hao wamesema utasaidia kuwarejesha watu walioacha kutumia dawa na ambao wanakwepa kupima virusi vya ukimwi. 

Awali akifungua mafunzo hayo kaimu mganga mkuu mkoa wa Njombe Dr. David Ntahindwa kwa niaba ya mganga mkuu amesema ujuzi wanaopatiwa mawakili tiba ama waviu katika mafunzo hayo utumike kama muongozo wa mapambano dhidi ya ugonjwa wa ukimwi kuanzia ngazi ya chini kabisa ya jamii.  

Mradi huo unatarajiwa kutekelezwa kwa muda wa miaka mitano ambapo katika kanda ya mbeya umehusisha washiriki kutoka mikoa ya mbeya, Njombe na iringa.

Post a Comment

0 Comments