TANGAZA NASI

header ads

Corona:Diwani ashangaa wanaosubiri serikali itangaze kufunga makanisa





Na Amiri kilagalila,Njombe

Mwenyekiti wa halmashauri ya mji wa Njombe Edwin Mwanzinga ambaye pia ni diwani  (CCM) kata ya Matola ameshangazwa na watu wanaosubiri serikali kutangaza kufunga makanisa wakati tahadhari dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona (COVID-19) zilikwishatolewa.

Mwanzinga amesema anaamini wananchi wanaelewa taratibu za kujikinga dhidi ya virusi hivyo ikiwemo kuepuka mikusanyiko lakini anashangazwa kuona watu bado wanakwenda makanisani wakisubili serikali kufunga makanisa.

Ameyasema hayo mbele ya waandishi wa habari walipofika ofisini kwake ili kupata maoni upatikanaji wa vifaa muhimu vya kujikinga na Corona hususani Barakoa kwa mji wa Njombe hasa katika kipindi hiki cha mlipuko.

“Mimi ni imani yangu kubwa kwamba wananchi wanaelewa tahadhari kwamba mikusanyiko haitakiwi,sasa wewe unaenda kwenye baa ,kwenye mikusanyiko kufanya nini? kama unaamini kabisa kanisani kuna mkusanyiko kwanini usikae nyumbani kwako ukaomba,sasa wanataka serikali mpaka itangaze kufunga makanisa,kufunga masoko”alisema Mwanzinga

Kuhusu swala la Barakoa Mwanzinga amesema inawezekana ikawa ni changamoto kwa kuwa awali hazikuwa na matumizi makubwa mitaani.

“Kwanza mwanzo hatukuwa na hivyo vitu na kama vilikuwepo basi walikuwa wanavaa walioko kwenye fani ya afya au kilimo ndio walikuwa wanavaa barakoa,lakini sahizi nimeona nyingi hata za kawaida zinatengenezwa kwasababu swala ni kuzuia mate yako unapoongea yasiruke kwa mwenzangu,na ninadhani wafanyabiashara kwa sasa wameanza kuziingiza kwa wingi”alisema Mwanzinga

Winfrida Mtete Onesmo Mwajombe na Stanley Nyatto ni Baadhi ya wakazi wa Njombe mjini ambao wengine wamekutwa  wakiwa wamevalia Barakoa na wengine wakisema muda bado kwa Njombe kuanza kuzivaa.

Wauzaji wa maduka makubwa ya dawa mhimu za binadamu mjini Njombe akiwemo Prisca Mwanyika wanakiri kuwapo kwa uhaba wa vifaa vya kujikinga na Corona Kama Hand sanitizer,Barakoa na sabuni na kwamba kutokana na mikoa Jirani ya Ruvuma na Mbeya kuripotiwa visa vya wagonjwa wa homa ya mapafu uhitaji wa vifaa hivyo umeanza kuwa mkubwa.

“Sisi tunaomba tupunguziwe bei hizi barakoa kwasababu upatikanaji wake ni mgumu sisi tunapata kidogo kidogo kwasababu ukitaka mia mtu anakupa 30 anasema hazitoshi anauza reja reja yeye mwenyewe,na sasa hivi boksi moja lenye barakoa 50 zinauzwa laki moja laikini uhitaji wa wateja hapa Njombe ni mkubwa tunashindwa sisi na serikali yetu isiangalie upande mmoja huku kusini tunasahaulika”alisema Prisca Mwanyika

Ripoti za wagonjwa wa Corona Nchini  kutokana na taarifa ya wizara ya afya Tanzania hadi sasa wagonjwa wanaotokana na virusi vya Corona wamefikia  254,vifo 10 na waliopona  ni 11.

Post a Comment

0 Comments