TANGAZA NASI

header ads

Mbunifu mwingine azalisha umeme Njombe asaidia wananchi zaidi ya 2700 kwa bei nafuu





Na Ibrahim Mlele,Njombe

Zaidi wananchi 2700 kijiji cha Havanga halmshauri ya wilaya ya Njombe wameanza kunufaika na mradi wa umeme uliobuniwa na Frank Kihombo mkazi wa kijiji cha Nyombo baada ya kuikosa nishati hiyo kwa muda mrefu.

Wakizungumza na kituo hiki kijijini hapo wananchi hao wameshukuru mbunifu huyo kwa kujitokeza kuanzisha mradi huo ambao unawasaidia katika matumizi mbalimbali ikiwemo kupata mwanga na kupata taarifa kupitia televisheni na radio.

“Tunanufaika kwa mambo mengi sana kupitia huu umeme mfano mimi ni fundi simu kuna baadhi ya vitu tulikuwa hatuvitumii kulingana na umeme haukuwepo lakini safari hii tunavitumia kwasababu umeme upo”alisema  Alex Kapinga moja ya mwananchi fundi umeme kijijini hapo

Mbunifu huyu anasema hana taaluma ya ufundi wa umeme ila amekuwa na kipaji tangu alipozaliwa na alihamasika kuanzisha mradi katika kijiji hicho baada ya kuona wananchi wanataabika ingawa mradi huo bado haujakamilika kutokana na kukosa vifaa mhimu zikiwemo nyaya.

“Nilipofika hapa nikakutana na maji ya kutosha na wananchi wanaishi kwa kutumia solar,jua lisipowaka hawana mwanga nikaona wacha niwasaidie nitengeneze huu umeme ili waweze kupata nuru” Frank Kihombo

“Niliona nitengeneze huu umeme watu wapate nuru wakati huo nikionesha kipaji change kwamba ndoto zilizokuwa zinanitesa nionekane nilisaidia watu”aliongeza  Frank Kihombo
Vile vile ameomba serikali kupitia shirika la umeme Tanesco kumsaidia miundombinu

“Ninaomba wanisaidie miundombinu ambayoninakosa kwa mfano waya,nguzo baadhi ya mitambo ninayo transfoma za kusuka ninaweza za ukubwa wowote ule lakini kuna vifaa vingine sina uwezo navyo na pesa kwa sasa sina” Frank Kihombo

Serikali ya kijiji cha Havanga kupitia mtendaji wake Philimoni Lulimo imesema iliitisha kikao baada ya mbunifu huyo kujitokeza katika kuanzisha mradi na wameshirikiana naye kwenye baadhi ya shughuli na kwamba mradi huo umekuwa ni sehemu ya kuchochea maendeleo.
   
“Sasa hivi umeme huu unasaidia kwa maana ya matumizi ya kawaida majumbani na kwenye taasisi watoto wetu wa shule ya msingi wanapata neema ya kusoma hata usiku bila ya kuwa na kikwazo” alisema Philimoni Lulimo
Miezi kadhaa iliyopita kadhalika mkoa Njombe ulifanikiwa kuibuliwa wabunifu watatu kutoka vijiji tofauti hali iliyopelekea Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt,John Pombe Magufuli kuagiza wataalamu mbali mbali wakiwemo kutoka Tanesco kuwasaidia wabunifu hao kutokana na huduma wanazotoa kwa jamii.


Post a Comment

0 Comments