TANGAZA NASI

header ads

Madiwani waiagiza harmashauri kurekebisha sheria ya tozo

 



Na Amiri Kilagalila,Njombe

Baraza la madiwani halmashauri ya wilaya ya Njombe limeagiza ofisi ya mkurugunzi kufanyia marekebisho ya  sheria ya tozo ya ushuru wa mbao na mkaa ili kuvutia wafanyabiashara wengi  pamoja na wale ambao wamefika hatua ya kuhama kufanyabiashara katika halmashauri hiyo.

Katika mkutano wa baraza la madiwani halmashauri ya wilaya ya Njombe baadhi ya madiwani akiwemo Javan Ngumbuke na Roida Wandelage wamesema kumekuwapo kwa baadhi ya wafanyabiashara wanaotoroka kununua mbao na mikaa katika maeneo yao kutokana na tozo kubwa jambo linalokwamisha jitihada za ukusanyaji mapato.

“Watu wengi wanalalamika kwamba ushuru ni mkubwa na hata hapa Mtwango tulikuwa na wafanyabiashara wengi wa mbao sasa kwasababu ya ushuru mkubwa wamehama wanaenda knunua mbao halmashauri ya mji na wengine wameacha kabisa biashara hiyo na kuingia kulima mahindi wanadai ni bora kulima mahindi kwasababu ushuru ni naafuu kuliko ushuru wa mbao”alisema Roida Wandelage

Mwenyekiti wa halmashauri hiyo Valentino Hongoli amesema licha ya kufanikiwa kuvuka lengo katika makusanyo ya ndani lakini tozo kubwa zilizowekwa kupitia sheria ndogondogo zimesababisha baadhi ya wafanyabiashara wa mbao na mkaa kukimbilia katika halmashauri nyingine jambo ambalo ni lazima kubadilishwa kwa kanuni za tozo hizo.

“Kwa kuwa kilimo cha wafanyabiashara wetu wa mbao na mkaa ni kuwa halmashauri yetu tunachaji ushuru mkubwa mno tofauti na halmashauri nyingine,Niagize kupitia baraza hili kwako wewe na CMT yako mfanye mchakato wa haraka ili tuweze kufanya marekebisha ya hiyo sheria kwasababu ikifanyiwa marekebisho itawavutia wafanyabiashara wengi kuingia kununua mbao na mkaa katika halmashauri yetu hali ambayo itapandisha sana kupunguza na watu kukwepa mapato”alisema Valentino Hongoli

Kwa niaba ya mkuu wa wilaya ya Njombe,katibu tawala wa  wilaya hiyo  Emmanuel George amesema pamoja na jitihada kubwa zinazofanywa katika ukusanyaji mapato ya ndani lakini fedha hizo zisaidie katika kukamilisha maboma yaliyojengwa kwa kushirikiana na wananchi.

“Tuhakikishe tunakusanya mapato ya kutosha ili yaweze kufanikisha shughuli zingine za serikali lakini pia tunapokusanya vizuri tuhakikishe tunapeleka fedha kwenye miradi hususani umaliziaji wa maboma maana yake tuanokusanya vizuri pia tunapeleka fedha kwenye miradi vizuru”alisema Emmanuel George

Baadhi ya wafanyabiashara wa mkaa na mbao akiwemo Juma Augustino na Isaya Kaduma wamesema tozo hizo zimewafanya kuporomoka kiuchumi kutokana na tozo hizo kutoendana na soko la bidhaa za misitu ya mbao kitaifa na kimataifa.

Kaimu mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Njombe bwana Lukelo Mshaura amekiri kupokea maagizo hayo na kwamba atakwenda kuyafanyia kazi.

“Tuhakiksha mchakato unapita katika maeneo yote yanayotakiwa kupita ili tuhakikishe tunakuja na kitu ambacho ni msaada kwa wananchi lakini pia tumeshaiona changamoto hiyo na kujikita pia kutafuta vyanzo vingine endelevu,sisi tumeupokea huo ushauri na kuufanyia kazi”alisema Lukelo Msahura

Halmashauri hiyo inatajwa kutoza ushuru wa shilingi 200 kwa kila ubao huku halmashauri zingine zikitoza shilingi 100.Hata hivyo licha ya changamoto hizo lakini katika makusanyo ya ndani halmashauri ya wilaya ya njombe imefanikiwa kuvuka lengo la makusanyo  kwa kukusanya zaidi ya asilimia 111.

Post a Comment

0 Comments