TANGAZA NASI

header ads

Waziri aiagiza OSHA kufanya tathmini ya maeneo ya kazi yenye ajali,magonjwa mengi

 



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu, Kazi,Vijana,Ajira na wenye Ulemavu, Jenista Mhagama ameagiza Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) kufanya tathmini ya maeneo ya kazi yanayoongoza kwa matukio ya ajali na magonjwa pamoja na kubainisha visababishi vyake ili kuwezesha uandaaji wa mkakati wa kudhibiti visababishi hivyo.

Ametoa agizo hilo alipokuwa akifungua kikao cha pili cha baraza la wafanyakazi wa OSHA kilichofanyika jijini Dodoma kwa lengo la kupitia bajeti ya mwaka 2021/2022.

“Taarifa iliyotolewa na Kaimu Mtendaji Mkuu inaonesha taasisi yenu imekuwa na mafanikio makubwa katika kipindi cha miaka mitano iliyopita ambayo yametokana na maboresho mbali mbali ambayo yamekuwa yakifanyika na serikali ikiwemo kuondoa baadhi ya tozo ambazo zilionekana kuwa kero.Hivyo, nawaagiza kuendelea kufanya kazi kwa weledi na uadilifu ili kuweza kufikia lengo letu la kupunguza ajali na magonjwa yatokanayo na kazi na kuleta ustawi wa Taifa letu,” alieleza Mhagama.

Post a Comment

0 Comments