TANGAZA NASI

header ads

ADEM Bagamoyo yawanoa vikali Walimu wapatao 284 wa Shule za msingi mkoa wa Pwani juu ya uthibiti ubora

 



Na Victor Masangu, Bagamoyo.

AFISA  Elimu wa Mkoa wa Pwani Hadija Mcheka amesema ni lazima Walimu Wakuu watambue wajibu wao wa kuhakikisha wanatekeleza  shughuli ipasavyo katika suala zima la utoaji wa elimu katika shule za Msingi, zinatekelezwa kikamilifu ili  watoto waweze kupata elimu bora na si bora elimu na kuzalisha wahitimu wenye maarifa.

Mcheka ameyabainisha hayo  mjini Bagamoyo wakati akifunga Mafunzo maalum ya Uthibiti Ubora wa Shule wa ndani kwa Walimu wakuu 284 kutoka Mkoa wa Pwani yaliyofanyika Katika Tasisi ya Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM) 

Alisema mafunzo hayo yamewaongezea umahiri katika uongozi, kusimamia, kufuatilia na kutathimini utekelezaji wa maelekezo ya Serikali ya kutoa huduma ya elimu vile inavyopaswakwa kufuata   miongozo inayotolewa na kwamba  pamoja na miongozo hiyo bado yamekuwa yakihitaji kupata mafunzo kama hayo ili kuboresha utendaji kazi. 

 Mcheka alisema, nia ya Serikali  ni kuendelea kuboresha mazingira ya utoaji wa elimu katika taasisi za elimu ikiwemo Shule za Msingi kama ilivyofanya. 

Post a Comment

0 Comments