TANGAZA NASI

header ads

Ndugai ataja kilipoipa ugumu CCM uchaguzi mkuu 2020



 Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai amekieleza chombo hicho cha kutunga sheria leo Alhamisi Februari 11, 2021 kuwa CCM kilipata wakati mgumu kwenye kampeni za uchaguzi mkuu wa Oktoba 25, 2021 kutokana na wanawake kutozwa tozo wanapojifungua.


Ndugai ambaye ni mbunge wa Kongwa amesema kuna haja ya kuangalia kwa kuwa wanachozungumza wabunge kina ukweli na walikiona kwenye kampeni hasa mkoani Tabora.

Kauli ya Spika ilifuatiwa na swali la nyongeza la mbunge wa Viti Maalum, Hawa Mwaifunga aliyehoji kama Serikali inajua kuwa katika baadhi ya hospitali wanawatoza Sh50,000 wanaojifungua watoto wa kiume na Sh40,000 wanaojifungua watoto wa kike.

"Naomba sana mlitazame hilo watu wa Serikali maana lilitusumbua sana kwenye kampeni na sasa mkoani Tabora, jambo hilo lazima mlitazame kwa namna yake," amesema Ndugai.

Post a Comment

0 Comments