Na Amiri Kilagalila,Njombe
Watuhumiwa 5
wanashikiliwa na jeshi la polisi mkoa wa Njombe kwa tuhuma za kuhusika na wizi
wa magari 6 yaliyopatikana mikoa tofauti yanayosadikika yametokana na ujambazi.
Kamanda wa polisi mkoa wa Njombe Hamis Issa amesema
wanashikilia gari 6 zilizoibwa katika maeneo tofauti huku watuhumiwa 5
wakiendelee kuwahoji juu ya kuhusika na tuhuma za wizi huo.
“Tulikuwa tunatafuta gari moja matokeo yake tumeweza
kukamata gari zingine 6 ambazo zinahusishwa na kuibwa maeneo mbali mbali katika
nchi yetu”alisema Kamanda Issa
Kamanda aewataja watuhumiwa hao kuwa ni pamoja na “Kuna
mshtakiwa maarufu Endrick Husein jina maarufu (Kimya kimya) huyu ni mkazi wa
Dar es salaam,Sudy Mwinyi mkazi wa Uyole Mbeya,Method Mkongwa mkazi wa
Njombe,Iman Phidelis mkazi wa moshi fundi magari pamoja na Timoth Nehemia mkazi
wa Mufindi hawa wanashirikina kuiba magari na kuyapokea”alisema Hamis Issa
Amesema gari wanazoshikiria ni pamoja na aina ya
Noah rangi ya silver iliyoibwa mkoani Mbeya,Gari aina ya Spacio iliyotoka
Silali mkoani Mara,Rava 4 iliyokamatwa mkoani Singida,Carina iliyopatikna mjini
Njombe.
Amewataka watanzania waliopotelewa na gari hizo
kufika mkoani Njombe na vielelezo ili waweze kutambua gari zao kwa kuwa kwa
sasa zipo mikononi mwa polisi.
0 Comments