TANGAZA NASI

header ads

Wananchi waomba kuungwa mkono ujenzi wa Zahanati

 



Makete

Wananchi wa kijiji cha Usagatikwa kata ya Tandala wilayani Makete mkoani Njombe wamewaomba viongozi watakaochaguliwa katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 28 mwaka huu kwa nafasi ya udiwani wa kata hiyo na ubunge wa jimbo la Makete, waweze kuwaunga mkono juu ya mpango wa ujenzi wa zahanati ya kijiji hicho.

Wananchi hao Akiwemo Sioni Sanga na Abigo Albon Sanga wametoa kauli hiyo wakati wakizungumza na kituo hiki ambapo wamesema kuna umuhimu mkubwa wa kijiji hicho kuwa na zahanati kutokana na umbali uliopo kufika katika hospitali ya Consolatha Ikonda ambayo kwa sasa ndiyo wanayoitegemea kupata huduma.

Mwl Linusi Ally Vangamea wa Shule ya Msingi Usagatikwa ameungana na wananchi wa kijiji kicho kulilia kuwepo kwa Zahanati Kijijini hapo ili Kuepusha Usumbufu kwa wanafunzi Kusafiri mpaka Kijiji cha Jirani kupata Huduma.

Afisa mtendaji wa kijiji cha Usagatikwa Bi.Lucy Valentino Lukinga amesema tayari wameshafyatua tofali na wanatarajia kuanza kuzichoma wiki ijayo huku akiwataka wananchi waendelee kushirikiana na viongozi wao ili waweze kufanikisha ujenzi huo.

Post a Comment

0 Comments