TANGAZA NASI

header ads

CCM Njombe waweka wazi ratiba ya mapokezi ya mgombea wao mwenza wa kiti cha Urais

 



Na Amiri Kilagalila,Njombe

Chama cha Mapinduzi CCM mkoa wa Njombe kimewatangazia wananchi ratiba na mapokezi ya makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh,Samia Suluhu Hassan,ambaye pia ni mgombea mwenza wa kiti cha Urais 2020 anayetarajia kupokelewa mkoani humo katika wilaya ya Ludewa September 18 akitokea mkoa wa Ruvuma.

Katibu wa siasa na uenezi wa Chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Njombe Erasto Ngole mbele ya waandishi wa habari amefafanua ratiba ya mapokezi wa kiongozi huyo wa kitaifa

“Mgombea mwenza wa kiti cha Urais Mh,Samia Suluhu Hassan ataingia kwenye mkoa wetu tarehe 18 mwezi huu wa tisa na atatokea Ruvuma kupitia wilaya ya Ludewa na tarehe 19 atakuwa kwenye mkutano mkubwa wa kampeni kwenye kata ya Mlangali” amesema Erasto

Ngole alisema tena

“Makamu wa Rais (Mgombea mwenza) tarehe 20 majira ya mchana atakuwepo wilaya ya Njombe na atafanya mkutano mmoja tarafa ya Lupembe eneo la Wanginyi kwa hiyo wananchi wote wa jimbo la Lupembe wajue Makamu wa Rais atafanya mkutano katika maeneo yote” alisema Erasto Ngole

Vile vile alisema Makamu wa Rais atamaliza kampeni mkoa wa Njombe kupitia wilaya ya Makete mkoani humo

“Tarehe  21 mwezi huu 9 Makamu wa Rais (Mgombea mwenza) atafanya mkutano mkubwa sana kwenye uwanja wa Sabasaba eneo la Iwawa,Makete mjini.Wananjombe wajue mkoa wetu utatembelewa na wagombea wa Chama chetu cha Mapinduzi kwa hiyo baada ya Samia tutawatangazia pia ratiba ya Mh,Rais” Erasto Ngole katibu

Aidha bwana Ngole ametangaza amewatangazia wananchi uzinduzi wa kampeni za siasa kimkoa utakaofanyika hapo kesho Septemba 9/2020

“Kesho tarehe 9 mkoa wa Njombe unafanya uzinduzi wa kampeni kimkoa,na uzinduzi huu utafanyika viwanja vya polisi halmashauri ya mji wa Makambako,Wanaccm wote tunatakiwa kuhudhuria sherehe hizi tukiwa katika mavazi ya Chama,na wasanii wote mkoa wa Njombe wanaalikwa na watapata nafasi ya kuburudisha” Erasto Ngole

Katika hatua nyingine ametoa wito kwa wanachama na viongozi kuendelea kutafuta kura kata kwa kata katika maeneo yao

“Huu ni muda wa kutafuta kura,tunaendelea kuwaomba wagombea wetu waendelee kufanya kampeni za ndani kwa kuwa ni muhimu sana,waende kwenye ngazi ya mashina kwa maana ya nyumba kwa nyumba,mtu kwa mtu ili tuweze kushinda kwa kishindo” alisema Erasto

Post a Comment

0 Comments