TANGAZA NASI

header ads

Waziri wa Viwanda na Biashara ashangazwa na ubunifu Njombe




Na Amiri Kilagalila,Njombe

Mjasiriamali Ruben Mtitu maarufu  Mzee Kisangani  Aliye Buni  kiwanda cha kufua vyuma kutokana na madini ya mawe ya chuma na makaa ya mawe mkoani Njombe amemshangaza Waziri wa Viwanda na Biashara, Inocent Bashungwa  Baada ya   kuanzisha kiwanda ambacho amesema kitakuwa  msaada kwa taifa katika kulahisisha kupatikana kwa mali ghafi mbalimbali.

Waziri Inocent Bashungwa amefika katika kijiji cha Mkiu, Kata ya Madope wilayani Ludewa akiwa ameongozana na ujumbe wa viongozi wa Wizara ya Viwanda na Biashara pamoja na Wizara ya Madini kuona kiwanda cha mbunifu huyo, kikiwemo chanzo cha kuzalisha umeme wa nishati ya maji.

“Lakini teknolojia ambayo mnaiihitaji ili jiwe ili itoe Chuma na sisi tuna taasisi,katibu mkuu Prof,Shemdoe tumekuja nae tuangalie changamoto mnazokabiliwa nazo hizo taasisi zifike hapa tuangalie ni namna gani mnaweza kuzalisha na mpate hela”alisema Bashungwa

Kutokana na ujumbe wa viongozi  wa Wizara ya viwanda kufika katika eneo ambalo kiwanda cha kutengeneza zana mbalimbali  kwa kutumia Madini ya mawe ya chuma  Mzee Rubeni Mtitu amezungumzia ujio wa waziri viwanda na Biashara Njombe

“Tunashukuru kwa ushirikiano pamoja na sisi” alisema Mzee Mtitu

Hata hivyo waziri  Bashungwa  kwa kushirikiana na Wizara ya Madini pamoja na Wizara ya Nishati ameahidi kuwa wataendelea kumuunga mkono mjasiriamali huyo ili uzalishaji wa bidhaa muhimu zitonakazo na chuma ziweze kuzalishwa kwa ingi  hapa nchini.

Katika kukamilisha ziara yake mkoani  Njombe bashungwa ametembelea kiwanda cha kusindika Parachichi cha Olivado kilichopo wilayani Wanging'ombe na kuwataka wananchi kuendelea kulima zao la Parachichi kwa kuwa serikali inaandaa miundo mbinu bora ya upatikanaji wa soko.


Post a Comment

0 Comments