Na Amiri Kilagalila,Njombe
Mkuu wa mkoa wa Njombe Mhandisi Mwita Marwa Rubirya,amewaagiza wakala wa
majengo Tanzania TBA mkoa wa Njombe kuongeza kasi ya ujenzi wa mradi jengo la
ofisi ya mkoa wa Njombe ndani ya siku kabla serikali kulazimika kusitisha
mkataba wao na kuandaa utaratibu mwingine wa ukamilishaji wa kazi hiyo ulionza
Oktoba, 2017.
Mkuu wa mkoa wa Njombe ametoa agizo hilo mara baada ya kukagua
maendeleo ya ujenzi wa jengo hilo linalojengwa Lunyanywi mjini Njombe na
kubaini udhaifu kwenye utekelezaji.
“Mkandarasi ni TBA ambaye alitakiwa awe amekamilisha kazi hii
June mwaka huu baada ya kukagua tumeona udhaifu mkubwa kwenye upande wa
utekelezaji,na vifaa ni vichache kama mnavyoona lakini hata watendaji
hawaridhishi”alisema Rubirya
Aidha Rubirya ameongeza kuwa
“Kwa hiyo tumetoa maelekezo kuwa TBA wahakikishe wanaleta vifaa
na wataalamu ili kuhakikisha kazi hii inakwenda kwa kasi ili tuweze kukamilisha
mradi huu na tumewapa angalizo wasipofanya kazi hiyo ndani ya siku saba kubadilisha
hali ya utendaji,tutalazimika kusitisha mkataba wao ili kuandaa utaratibu
mwingine wa kukamilisha kazi hii.
Kaimu meneja wakala wa majengo TBA mkoa wa Njombe Mhandisi Herman
Daudi Tanguye,amesema mradi wa ujenzi wa ofisi hizo unaoghalimu zaidi ya
bilioni 5.6 unakabiliwa na changamoto nyingi hivyo anaamini utakamilika Februal
17,2021 endapo taratibu za kifedha zitaendelea vizuri.
“Mradi una changamoto nyingi,jambo la kwanza ni upatikanaji wa
vifaa vya ujenzi kwa mfano mchanga unapatikana zaidi ya KM 60 kutoka eneo la
mradi na Njombe kuna mvua nyingi na jengo hili limejengwa eneo ambalo halina
barabara lakini tumewasiliana TARULA mara kadhaa ili angalau waweze
kutungenezea barabara”alisema Tanguye
Vile vile amesema Changamoto nyingine ni kutokana ugumu wa
upatikanaji wa kokoto zinazopatikana maeneo machache ikiwemo Chalinze mkoani
Pwani pamoja na uguu wa upatikanaji wa Mafundi na vibarua ambao mara kwa
wamekuwa wakipatikana wilaya za jirani ambao wamekuwa wakishindwa kufanya kazi
kulingana na mazingira.
Aidha amesema wamepkea maelekezo ya mkuu wa mkoa wa Njombe na
kuhakikisha ndani ya kipindi hicho yanatekelezwa.
0 Comments