TANGAZA NASI

header ads

CHADEMA watangaza kutikisa kwa kuweka wagombea wa ubunge majimbo yote 6 Njombe



Na Amiri Kilgalila,Njombe

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema mkoa wa Njombe Rose Mayemba,amesema chama hicho kimejipanga kuweka wagombea wa  ubunge katika majimbo yote ya uchaguzi mkoani Njombe
Rose  ameyasema hayo mkoani Njombe wakati wa mahojiano na kituo cha Radio King’s kilichopo halmashauri ya mji wa Njombe mkoani humo

“Wananchi wajitokeze kuwasikiliza pale ambapo tutakuwa tumeanza mtanange,tunawagombea  katika majimbo yetu yote sita  na ni wagombea wazuru tunaamini mambo yatakuwa mazuri” Rose Mayemba Mwenyekiti Chadema Njombe

Vile vile Rose amesema

“Chadema mkoa wa Njombe tumejiandaa na tunawagombea wa kutosha,tuna kata 107 lakini tunawagombea karibu kila na ni mkakati kwamba hakuna kata itakwenda kwenye uchaguzi bila kuwa na mgombea” Rose Mayemba Mwenyekiti Chadema Njombe

Mkoa wa Njombe una jumla ya majimbo 6 ya uchaguzi likiwemo jimbo la Njombe mjini,Makambako,jimbo la Ludewa,Makete,jimbo la Lupembe pamoja na jimbo la Wanging’ombe yote yakiongozwa na Chama cha mapinduzi CCM

Post a Comment

0 Comments