TANGAZA NASI

header ads

Polisi Morogoro wafungua kituo cha Polisi Mbingu




Na John Claud

Jeshi la polisi mkoani Morogoro limefungua kituo cha polisi Mbingu kilichopo wilaya ya kilombero baada ya wananchi kujichukulia sheria mikononi  kukichoma moto mwaka 2015 wakitaka kufanya jaribio la kumua mtuhumiwa aliefikishwa kituoni hapo na kisha jeshi hilo kufanikiwa kumtorosha.

Akizungumza na wananchi wa kijiji hicho kamishna msaidizi mwandamizi wa jeshi la polisi mkoani Morogoro Willbroad Mutafungwa amesema kuwa ameridhishwa na ujenzi wa kituo hicho licha ya kutokukamilika kwa asilimia  zote na sasa ni wakati muafaka wananchi wa kijiji hicho  kupata huduma za kipolisi huku mambo mengine yakiendelea kukamilishwa.

Katika hatua nyingine Kamanda Mutafungwa amewataka wenyeviti wa vijiji wilayani kilombero kuweka  utaratibu wa kuanzisha  kamati za ulinzi na usalama zitakazo wachagua vijana walio  waadilifu  ambao watakuwa ni sehemu ya ulinzi shirikishi na polisi jamii  ili kuimarisha  doria sehemu mbalimbali za maeneo yao.

Kwa upande wake mwenyekiti wa kijiji cha Mbingu Erasto Mgenda  amelishukuru jeshi la polisi kwa kukubali kuzindua kituo hicho kipya huku akiliomba kuwapatia askari waaminifu ambao watashirikiana na wananchi wa kijiji hicho.

Bahati Mwakagugu ni mkazi wa kijiji cha Igima amesema kuwa kwa muda wa mika mitano wamekuwa wakilazimika kutumia gharama kubwa kusafiri umbali mrefu  hadi kijiji jirani ili kupata huduma za kipolisi hasa yanapotokea matukio ya kihalifu.

Post a Comment

0 Comments