TANGAZA NASI

header ads

Afisa Mtendaji awawashia moto walioanza siasa chini chini



 Na Iganatio Cherls,Ludewa 

Ofisi ya Afisa Mtendaji kata ya Ibumi Tarafa ya Liganga Wilayani Ludewa Mkaoni Njombe imesema haitasita kuwakamata na kuwashughulikia kisheria wale wote wanaojihusisha na masuala ya kisiasa kabla ya muda uliopangwa kuanza shuhuli za uchaguzi.
 
Akitoa  Taarifa yenye tahadhari mbele ya wajumbe wa kamati ya maendeleo ya kata Ibumi Afisa mtendaji huyo wa kata Bw,Felix Charle  viongozi waliochaguliwa mwaka 2015 na kupewa dhamana ya kuongoza bado wanafanya kazi hivyo atakaye onekana anafanya kampeni zinazohusu uchaguzi atakamatwa.

Katika hatua nyingine  Bw,Charle ameongeza kuwa ni kosa la jinai mtu kufanya siasa kabla ya wakati kufika au Mamlaka husika hazijatoa maelekezo kwani kufanya hivyo kuikosea sheria ya uchaguzi.

Afisa Mtendaji huyo ametoa wito kwa kuwataka watanzania waendelee kufanya shughuli za kimaendeleo ili kukuza uchumi wa mtu mmoja mmoja,familia na Taifa

Post a Comment

0 Comments