TANGAZA NASI

header ads

Serikali yakamilisha adhma ya kuwa na benki moja mahsusi ya biashara




SERIKALI imekamilisha azma ya kuwa na benki  moja mahsusi ya biashara baada ya  kuunganisha benki zake mbili za biashara,benki ya Uwekezaji Tanzania(TIB Corporate Limited) na benki ya Posta Tanzania(TPB blank Plc).

Lengo la kufanya hivyo ni kuifanya benki kuwa imara,kuongeza ufanisi na kupunguza gharama za uendeshaji.

Akizungumza na waandishi wa  habari leo jijini Dodoma,Msajili wa hazina Athuman Mbutuka amesema muunganiko huo ni hatua mojawapo inayochukua zenye lengo la kuboresha utendaji wa mashirika na taasisi za umma.

Mbutuka amewahakikishia watanzania kuwa muunganiko huo hautaathiri huduma za kibenki.

Mei 26 mwaka huu Waziri wa Fedha na Mipango Dokta Philip Mpango aliweka bayana dhamira ya kuunganisha mifuko hiyo wakati akijibu hoja za wabunge walizozitoa wakati wa mjadala wa kamati ya kudumu ya bunge ya hesabu za serikali(PAC)kuhusu taarifa za mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali(CAG)zilizokaguliwa na serikali kuu na mashirika ya umma kwa mwaka wa fedha unaoishia mwezi juni 2020.

Pamoja na muunganiko huo serikali imewahakikishia wafanyakazi waliokuwa katika benki hizo kuwa ajira zao hazitaathirika.

Post a Comment

0 Comments