TANGAZA NASI

header ads

Makete DC wafanikiwa kupunguza hoja za mkaguzi



Na Henrick Idawa,Makete

Halmashauri ya wilaya ya Makete mkoani Njombe imepongezwa kwa kupata hati safi 2018/2019 na kupunguza hoja za mdhibiti na mkaguzi mkuu wa serikali CAG kutoka 44 zilizokuwepo na kubaki 24

Hayo yamebainika leo katika Baraza maalum la madiwani Halmashauri ya wilaya ya Makete lililokuwa na lengo la kujadili hoja za Mdhibiti na mkaguzi Mkuu wa serikali ambapo Katibu Tawala Mkoa wa Njombe Katarina Revocati ambaye amemuwakilisha mkuu wa mkoa wa Njombe ameonesha kufurahishwa na jambo hilo

Mbali na pongezi hizo pia ameitaka halmashauri hiyo kuhakikisha inasimamia vizuri ukusanyaji wa mapato na ihakikishe wakusanyaji wanafikisha mapato hayo ya serikali benki kama sheria inavyotaka ili kuepuka upotevu wa mapato

Naye Mkuu wa wilaya ya Makete Mh Veronica Kessy amekemea vitendo vya baadhi ya watendaji kufuja mapato ya serikali kwa kutumia fedha hizo kwa matumizi yao binafsi kinyume cha sheria

Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Makete Mh Egnatio Mtawa amemtoa shaka katibu Tawala wa Mkoa kwamba tayari wameweka utaratibu mzuri wa kuhakikisha mapato yakikusanywa yanafikishwa benki.

Diwani wa kata ya Mlondwe Mh. Alphonce Salim amesema upatikanaji wa hati safi kwa halmashauri ni jambo jema walilokuwa wakilitaka muda mtefu

Post a Comment

0 Comments