TANGAZA NASI

header ads

Ufaulu kidato cha nne umeongezeka-JPM



Na Jackline Kuwanda,DODOMA.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli amesema kuwa ufaulu katika shule za msingi na Sekondari umeongezeka.

Ufaulu wa Darasa la Nne umefikia asilimia 91.9%, Darasa la saba ukiongezeka kutoka 57 % mwaka 2015 hadi 81.5 % mwaka 2019 huku ufauli wa kidato cha nne ukiongezeka  kutoka 69.8% mwaka 2015 hadi kufikia 80.65% mwaka 2019.

Rais Magufuli ameyasema hayo Jijini Dodoma wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT),ambapo amewapongeza walimu kote nchini kwa kuwezesha kupatikana kwa mafaniko hayo kwani bila ya walimu kutoa ushirikiano huo mafaniko hayo yasingepatikana huku akisema kuwa ataendelea kuwalipa walimu mishahara yao licha ya kuwa shule zimefungwa kutokana na janga la corona.

Amesema walimu ndio wazalishaji wa sekta zote  hivyo hawana budi kutambua ,kuenzi na kuthamini mchango wa walimu katika nchi  huku akibainisha kuwa licha ya uwepo wa mafaniko katika sekta ya elimu lakini anatumbua kuwa zipo changamoto katika sekta hiyo ambazo zimeendelea kuwepo kwani serikali inazifahamu na inaendelea kuzishghulikia

Katika hatua nyingine Rais Magufuli amesema kuwa baada ya kufanyika kwa zoezi la uhakiki serikali tayari imewapandisha vyeo watumishi laki tatu na sita na mia tisa kumi na saba ambapo walimu wakiwa ni laki moja sitini elfu na mia tatu sitini na saba

Awali akisoma Risala mbele ya Mgeni Rasmi Katibu Mkuu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) Comred Mwalimu Deus Seif amesema kuwa chama kinatambua jitihada zinazofanywa na serikali katika kuboresha maisha ya watanzania ikiwemo walimu  kwani kwa upande wa sekta ya elimu  yapo mambo mbalimbali ambayo serikali imeyafanya kwa kipindi cha miaka mitano ikiwemo ongezeko la miundombinu na samani,upandishaji wa madaraja na marekebisho ya mishahara kwa walimu huku akibainisha changamoto zilizopo licha ya mafaniko yaliyopo.

Akizungumza kwa niaba ya walimu wote Nchini Tanzania Rais wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) Leah Ulaya amempongeza Rais Magufuli kwa kuendelea kuenzi tasinia ya ualimu kwani amehakikisha kuwa mahitaji yote muhimu walimu yanapatikana.

Kwa upande wake Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Bunge,Vijana,Ajira na wenye ulemavu Mh Jenista Mhagama amelipongeza shirikisho la vyama vya wafanyakazi na viongozi wake hapa nchini kwa kuwa viongozi imara kwani wameweza kuongeza vyema vyama hivyo.


Post a Comment

0 Comments