TANGAZA NASI

header ads

Ludewa:Wananchi waomba barabara



Na Amiri Kilagalila,Njombe

Wananchi wa kitongoji cha Mking’ino kijiji cha Luvuyo kata ya Madope wilayani Ludewa mkoani Njombe wameiomba serikali kuboresha miundombinu ya barabara inayounganisha kijiji chao na vijiji  jirani ili kurahisisha upatikanaji wa huduma mbalimbali za kijamii.

Wakazi hao akiwemo Erasto Mtega, Junitha Mbukwa na Stia Chaula wamesema asilimia kubwa ya wakazi wa eneo hilo ni wakulima wa mazao ya viazi mviringo na mahindi lakini changamoto ya ubovu wa barabara inawalazimu kuuza mazao yao kwa bei ya chini tofauti na maeneo mengine.

“Mfano muda wa masika tunapata tabu sana kwenye usafirishaji,tunweza tukalima mahindi lakini yanaozea shambani kwa kushindwa kusafirisha,tunaomba Mh,Rais  aangalie kwa jicho lingine”alisema Stia Chaula

Aidha wamesema licha ya kuwa jirani na kata za Lupanga na Mlangali zilizopo wilayani Ludewa lakini kitongoji cha Mking’ino hakina barabara ya uhakika inayoelekea kwenye maeneo hayo jambo ambalo limekuwa likisababisha wakazi wa eneo hilo wakiwemo akina mama na watoto kupata shida ya kufuata huduma za afya pindi wanapo ugua.

Licha ya kukiri uwepo wa changamoto ya ubovu wa barabara katika baadhi ya maeneo ya kata ya Madope diwani mstaafu wa kata hiyo  Policap Mlelwa amesema serikali kupitia wakala wa barabara za mijini na vijijini tarura wilayani Ludewa imeanza kuboresha baadhi ya barabara hizo ikiwemo ya kutoka kijiji cha Madope kuelekea Luvuyo.

“Ninahakika kwamba wananchi wangu wa Mking’ino wanachangamoto ya barabara,lakini kwa mara ya kwanza tumeifikisha eneo Fulani kwa kutengeneza kwa gleda ila kwasababu ya mvua ile barabara bado ni mbaya,lakini kwasababu fedha tuliyoipata inaishia inaishia Luvuyo ninaimani 20/21 tutakwenda mpaka Mking’ino na barabara ile tumeijenga KM 3 kwa kokoto lakini inaendelea kuboreshwa”alisema Mlelwa

Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dokta John Pombe Magufuli imejipambanua wazi katika kufanyakazi ikiwemo kuelekeza nguvu kubwa katika sekta ya miundombinu lakini wakazi hao bado wanalia na changamoto ya barabara.



Post a Comment

0 Comments