TANGAZA NASI

header ads

Tani zaidi ya 100,000 za mazao mbalimbali kutoka kwa wakulima wa ndani zimenunuliwa na kuuzwa nje ya Nchi




Dodoma. 

Zaidi ya tani 100,000 za mazao mbalimbali kutoka kwa wakulima wa ndani zimenunuliwa na kuuzwa kwenye nchi za Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Sudan Kusini kupitia bodi ya nafaka na mazao mchanganyiko.

Akitoa taarifa hiyo jijini Dodoma mkurugenzi mkuu wa bodi ya nafaka na mazao mchanganyiko  DK  Anselim Mushi amesema biashara hiyo imefanyika kwa kipindi cha miezi minne iliyopita na kutengeneza Serikali faida ya zaidi ya Sh3.2 bilioni.

DK Mushi amesema bodi hiyo inatarajia kununua tani za ziada 300,000 kwa ajili ya kuziuzia katika nchi za Afrika Mashariki.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Kilimo Omary Mgumba amesema hatua hiyo imeongeza soko la uhakika kwa wakulima huku akiitaka bodi ihakikishe kunakuwepo na usalama wa chakula nchini.

Mbali na Naibu Waziri Mgumba kuitembelea bodi hiyo pia ametembelea kituo cha utafiti wa kilimo cha Hombolo jijini Dodoma na kujionea uzalishaji wa mtama, uwele na zabibu mazao ambayo yanayostahimili ukame.

Post a Comment

0 Comments