TANGAZA NASI

header ads

Mwenyekiti UWT aonyesha njia,adai chanjo ni salama,aomba wanawake wakachanje kuokoa familia


 


Na Amiri Kilagalila,Njombe

Wananchi mkoani Njombe wametakiwa kujitokeza kwa wingi kupata chanjo ya UVIKO 19 inayotolewa kwenye vituo mbalimbali vya afya vilivyoainishwa kwakua haina madhara yeyote.

Kauli hiyo imetolewa na mwenyekiti wa umoja wa wanawake chama cha mapinduizi UWT mkoa wa Njombe Scolastika Klistiani Kevela baada ya yeye mwenyewe kuchanja katika kituo cha afya kibena.

"Mhe,Rais ametuambia kwamba kuchanjwa ni muhimu kwa ajili ya afya zetu na ni hiari mimi nimejitokeza leo kuchanja kuonyesha kwamba chanjo ni muhimu kwa ajili ya afya zetu"alisema Scolastika Kevela

aliongeza kuwa "Mtu aliyechanja na asiyechanja tofauti yake ni kwamba wewe ambaye hujachanja Covid 19 ikikukuta ni rahisi kukuchukua,mimi niliyechanja nakuwa na asilimia ndigo ya kuathirika"

Katika hatua nyingine mwenyekiti huyo amewataka wananchi kupuuza baadhi ya maneno ya watu ambao wanazusha kuhusu chanjo bali wamuunge mkono Mh,Raisi Samia Suluhu Hassani kwakua nae ameshachanja.

"Ninawaambia wananchi wa mkoa wa Njombe na wakina mama wajitokeze kwa wingi kupata hizi chanjo kwa ajili ya usalama wa maisha na familia zao"aliongeza Scola

Nao baadhi ya wananchi waliopatiwa chanjo akiwemo bwana Bunduki na Mwalongo maarufu kwa jina la kakuku wamesema wanajisikia furaha kuchanja na hawajapata changamoto yeyote kiafya.  

"Nilipofika hapa haikuchukua hata dakika 10 kwenye kituo nikawa nimeshachanja kwa kuwa watu ni wachache na ni bora watu wakapata chanjo kuliko homa ikakuzidia"alisema Kakuku

Post a Comment

0 Comments