Na Amiri Kilagalila,Njombe
Jeshi la polisi mkoani Njombe linawashikilia walimu
wawili wa shule ya sekondari Mang’oto wilayani Makete mkoani Njombe,kwa tuhuma
za kumsababishia ujauzitoa na kumtoa mwanafunzi wa shule hiyo mwenye umri wa
miaka 17.
Akizungumza na vyombo vya habari,kamanda wa jeshi la
polisi mkoa wa Njombe Hamis Issa,amesema wanamshikilia mwalimu Ezekiel Thomas
(36) maarufu kwa jina la Dokole,kwa kuwa na mahusiano na mwananfunzi na
kumsababishia ujauzito.
“Huyu mwalimu amekuwa na mahusiano na mtoto wa
sekondari mwenye umri wa miaka 17 na binti huyo amepimwa amegundulika ni mjamzito”alisema kamanda Issa
Aidha amesema wanamshikilia mwalimu Ben Liamdilo
(35) kwa kushirikiana katika tukioa la utoaji wa mimba na kumsababishia maumivu
mwanafunzi.
“Mwalimu Thomas alifanya juhudi akamtuma huyu
mwalimu mwenzake akambeba na boda boda kwenda kumtoa mimba mpaka sasa hivi
walimu wote wawili tunawashikilia na wanatuhumiwa na makosa haya”alisema tena
kamanda Issa
Vile vile ameitaka jamii kushirikiana kwa kutoa
taarifa kwa jeshi la polisi ili kukabiliana na vitendo kama hivyo.
0 Comments