Na Amiri Kilagalila,Njombe
Waziri
wa nchi Ofisi ya Rais tawala za mikoa na serikali za mitaa, (TAMISEMI)
Mheshimiwa Selemani Jafo amewaagiza wakurugenzi wote wa halmashauri 185 nchini
kuhakikisha wanafikisha zaidi ya 50% ya makusanyo ya mapato ifikapo Januari
15,2021
Ametoa
agizo hilo wakati akiwasalimia watumishi wa halmashauri ya mji wa Njombe katika
ukumbi wa halmashauri hiyo akipita kuelekea mkoani Ruvuma huku akiwataka watakaoshindwa
kufika nusu ya lengo wajitafakari
“Tarehe
15 mwezi wa kwanza nitatoa taarifa ya miezi 6 ya ukusanayaji mapato,wakurugenzi
wote wa halmashauri 185 wakajipime wakati wanaenda krismasi sitaki kuona
halmashauri yoyote iliyopata chini ya 50%”alisema Waziri Jafo.
Jafo
aliongeza kuwa “Halmashauri itakayokuwa imekusanya chini ya 50% mkurugenzi huyo je anafaa kuendelea na serikali ya awamu
ya pili ya kipindi cha tano cha Dkt,John Pombe Magufuli ama hatoshi awekwe
pembezoni aje mwingine anayeweza kukusanya mapato”aliongeza Jafo
Amesema
“Hatutashughulika na wakurugenzi peke yake tutashughulika na watunza hazina
pamoja na maafisa mipango,hili ni agizo langu kwa halmashauri zote nchi nzima
Aidha
waziri Jafo ameipongeza halmashauri ya wilaya ya Njombe na mkurugenzi wake
Bwana Ally Juma kwa kufanikiwa kuongoza katika taarifa yake iliyoishia jana 21
Disemba ikionyesha halmashauri hiyo kuongoza kimkoa na kuwa miongozni mwa
halmashauri inayofanya vizuri kitaifa.
“Naipongeza
halmashauri ya wilaya ya Njombe ambayo mpaka jana tarehe 21 Disember kwenye
taarifa yangu wamekusanya bilioni 1.707 sawa na 72% na ni miongoni mwa halmashauri mpaka leo zilizokuwa
kinara Tanzania kwa ukusanyaji wa mapato”alisema Seleman Jafo
Hata
hivyo amesema halmashauri ya wilaya ya Makete ndiyo inayofanya vibaya mpaka
sasa katika mkoa wa Njombe kwa kukusanya milioni 599
“Taarifa
yangu mpaka jana inaonyesha halmashauri ya wilaya ya Makete imekusanya milioni
599 sawa na 25% nje ya bilioni 2.441kwa
hiyo mna kazi kubwa ya madeni”alisema Jafo
“Halmsahauri
ya mji wa Njombe imekusanya 48% mpaka jana 21 Disemba sawa na 3.299 bilioni
tunapomaliza mwezi huu disemba tunatarajia halmashauri zote ziwe zimekusanya
sio chini ya 50%”alisema waziri Jafo
Mbunge
wa jimbo la Njombe mjini Mh,Deodatus Mwanyika amemshukuru waziri Jafo kwa
kufika katika halmashauri hiyo na kukagua baadhi ya miladi inayojengwa ndani ya
halmashauri ya mji wa Njombe
0 Comments