TANGAZA NASI

header ads

Mlangali wafikisha wajawazito 50 kwa Mwezi

 



Na Amiri Kilagalila’Njombe

Kituo cha afya Mlangali wilayani Ludewa mkoani Njombe kimefanikiwa kuanza kupokea karibu wajawazito 50 kutoka 15 wa awali kwa mwezi,kutokana na kuimarishwa kwa huduma za afya na uboreshaji wa majengo uliofanywa na serikali ya awamu ya tano.

Mganga mkuu wa kituo hicho cha afya kata ya Mlangali Dkt,Rebeca Mduma amewaeleza waandishi wa habari kuwa awali kituo kilikuwa kikipokea wajawazito wachache kutokana na akina mama wanaohitaji kupata huduma kuelekea katika vituo vingine vinavyotoa huduma zinazokidhi mahitaji ya wajawazito.

“Awali kwasababu ya miundombinu mibovu walikuwa wanafika wamama wajawazito lakini ilkuwa inabidi tuwafikishe hospitali ya jirani,lakini sasa haya majengo yamesaidia mpaka tumeongeza huduma, baada ya huduma kupanuka na majengo kuongezeka tumeona hata kilinki akina mama wameongezeka wakati ninafika walikuwa wanafika 15 kwa mwezi lakini sahizi tumefika karibia hamsini”alisema Dkt,Rebeca Mduma

Aidha amesema licha ya kufanikiwa kupata vifaa mbali mbali vinavyokidhi mahitaji ya kituo pamoja na majengo mapya laikini bado wanakabiliwa na changamoto ya wauguzi pamoja na umeme.

“Changamoto nyingi zimetatuliwa na  serikali iliopo lakini bado wauguzi ni wachache na uongozi wa wilaya uliongeza wahudumu baada ya sisi kuanza huduma hizi nyingine lakini pia changamoto zingine kituo kimekuwa kikubwa lakini kunachangamoto ya umeme ambao tumekuwa tukipata kwa mgao”aliongeza Dkt,Rebeca Mduma

Merry Mapunda ni mwalimu mstaafu na Gervas Mwinuka ni muuguzi mstaafu wanaoishi kijiji cha Itundu kata ya Mlangali.Wanasema kituo cha afya Mlangali kimekuwa na maendeleo makubwa kwenye utoji wa huduma za afya.

“Tumepata wataalamu bora zaidi ambapo zamani tulitegemea vituo vingine lakini laeo tunafanyiwa hapa hapa na toka lianze zoezi hili hatujaskia mama aliyepasuliwa akafa”alisema Merry Mapunda

Katibu wa siasa na uenezi wa Chama cha Mapinduzi mkoa wa Njombe Erasto Ngole akiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa Ilani ya Chama hicho amefika na kukagua utoaji wa huduma katika kituo hicho na kuridhishwa na watumishi jinsi wanavofanya kazi huku akiahidi kutoa mchango wake wa kitanda kimoja kwenye wodi la mama na mtoto huku akichukua changamoto zingine na kuzifikisha katika mamlaka zingine.

“Tumeona huko ndani vifaa tiba vya kutosha lakini watumishi wa kutosha,na watumishi wa hapa hawalalamikiwi na wananchi hiyo ni miongoni mwa mikakati ya Magufuli aliyoisimamia kwa maana ya kuleta nidhamu serikalini”alisema Ngole

Vile vile Ngole amefika na kukagua maendeleo ya ujenzi wa barabara ya Njombe-Ludewa kipande cha Lusitu-Mawengi inayojengwa kwa kiwango cha zege na kuridhishwa na kasi ya ujenzi.

Post a Comment

0 Comments