TANGAZA NASI

header ads

CCM yaridhishwa na ujenzi wa Barabara mkoani Njombe

 



Na Amiri Kilagalila,Njombe

Wananchi mkoani Njombe wameeleza kufurahishwa na ujenzi wa barabara za Njombe -makete kwa kiwango cha lami na ile ya Nyigo -Igawa zenye urefu wa takribani kilomita 171 na kugharimu mabilioni ya fedha ambazo ni kodi za watanzania.

baadhi ya wakazi hao akiwemo Adebayo Salum na Zakayo Mbwilo toka Moronga Njombe wanatoa kauli hiyo wakati wa ziara ya chama cha mapinduzi CCM mkoa wa njombe kupitia ofisi ya siasa na uenezi ilipofanya ukaguzi wa ujenzi wa barabara hizo ambao wamesema kwenda kukamilika kwa miradi hiyo kutakuwa fursa kwao kwa kuwa kumekuwa na adha kubwa ya usafirishaji mizigo wakati wa masika na hata gharama kubwa ya nauli kwenye mabasi.

“Barabara hii awali ilikuwa mbovu sana na ilkiuwa haipitiki kifuku lakini pia mazao yalikuwa hayatoki vizuri na bei ilikuwa ndogo,kwa hiyo sisi tunaishukuru sana serikali kwa kutuona”Alisema Adebayo Salum

Erasto Ngole ni katibu wa siasa na uenezi CCM mkoa wa Njombe wakati akikagua ujenzi wa barabara hizo amewataka wakazi wa Makete kutumia barabara hizo kama fursa kwao katika kujiletea maendeleo na kutakiwa kurudi kuwekeza sasa.

“Mwaka 2015 tuliwaahidi watanzania kwamba barabara ya Njombe-Makete  na baadaye barabara ya Makete kuelekea Mbeya,mitambo mnayoiona ipo kazini na utekelezaji unaendelea,tunategemea barabara hii ndani ya miezi mitatu iwe imekamilika” alisema Erasto Ngole katibu wa siasa na uenezi mkoa wa Njombe

Ngole aliongeza tena

 “Wana Njombe na wana Makete tutumie fursa hii ya kupata barabara kutoka kwa Mh,Magufuli kwa kufanya kazi zaidi kwa kuwa tunakwenda kuifungua wilaya ya Makete na sasa muda Umefika kwa wanamakete kuja kuwekeza kwasababu miundombinu sasa ni rafiki” alisema Erasto Ngole katibu wa siasa na uenezi mkoa wa Njombe

Akikagua matumizi ya barabara ya Nyigo- Igawa,kutoka Makambako kuelekea mkoani Mbeya iliyoanza kutumika mara baada ya kuzinduliwa na Rais Magufuli mwishoni mwa mwaka uliopita, yenye urefu wa kilomita 64.6 kwa gharama zaidi ya shilingi bilioni 103 bwana Ngole amewataka wananchi kutunza miundombinu hiyo huku akilitaka jeshi la polisi lenye wajibu wa kulinda raia na mali zao kufanya ukaguzi wa mara kwa mara katika barabara hizo.

Barabara hizo zimetakiwa kutumika vyema na wakazi wa mkoa wa njombe na mataifa mengine katika kuwaingizia uchumi na pato la taifa kwa ujumla.

Post a Comment

0 Comments