TANGAZA NASI

header ads

Jeshi la ulinzi wa wananchi Kikosi cha Makambako watoa misaada kituo cha walemavu wa viungo

 



Na Amiri Kilagalila,Njombe

Katika kuadhimisha miaka 56 ya jeshi la ulinzi wa wananchi Tanzania hii leo Septemba 1,2019. Kikosi cha 514 Makambako kimetoa msaada wa vitu mbali mbali katika kituo cha kutibu watu wenye ulemavu wa viungo cha Inuka wilayani Wanging’ombe mkoani Njombe Pamoja na kuchangia damu katika kituo cha afya cha Jeshi mjini Makambako.   

Meja Iddi Sechonge  kaimu kamanda kikosi cha jeshi la ulinzi wa wananchi  kikosi cha 514 Makambako akikabidhi misaada hiyo katika kituo cha Inuka amesema kuwa jeshi linaadhimisha kuanzishwa kwake kwa kutoa misaada katika jamii inayolizunguka ili kuwasaidia wasiojiweza.

“Tunaadhimisha kuanzishwa kwa jeshi letu,kwa maana tumeona tushehereke na kituo hiki kwa ajili ya kuwapa chochote,lakini kuna wenzetu wanaendelea na zozi la kuchangia damu”alisema Meja Iddi Sechonge  

Kaimu mkurugenzi wa kituo cha Inuka Dokta Salehe Abdalaha amesema kuwa jamii bado inaimani potofu dhidhi ya watu wenye ulemavu Pamoja na kueleza kuwa misaada zaidi inahitajika kwa kuwa baadhi yao hushindwa kumudu gharama za matibabu.

“Kuna changamoto ya uelewa kwenye jamii na baadhi yaw engine wanadhaani ni laana lakini sisi tunachosema mtu anaweza akapata uleamvu saa yoyote”alisema Dokta Salehe Abdalaha

Zaidi ya uniti 35 za damu zimepatikatikana katika kituo cha afya cha jeshi la ulinzi wa wananchi   kikosi 514 Makambako Mkoani Njombe

Post a Comment

0 Comments