TANGAZA NASI

header ads

Makambako mbioni kuondokana na changamoto ya maji

 



MAKAMBAKO

Wakazi mjini Makambako mkoni Njombe wanataraji kuondokana na changamoto ya uhaba wa maji ifikapo Octoba mwaka huu baada ya serikali kupitia mamlka ya maji mjini humo MAKUWASA kukamilisha ujenzi wa mradi wa bwawani ulionza kujengwa tangu mwaka 2017 pamoja na tank la maji la lita laki moja.

Hayo yamebainishwa na Eng Fabiani Maganga msimamizi wa miradi ya maji inayojengwa kutika mikoa ya njombe na Iringa wakati kamati ya kusimamia miradi hiyo kutoka mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira ya mjini iriga IRUWASA ikiwa katika ziara ya kukagiua miradi hiyo katika mkoa wa Njombe.

Mkurugenzi wa mamlaka ya majisafi na usafi wa mazingira mji wa makambako MAKUWASA Osca Lufyagile amesema kuwa kukamilika kwa mradi huo kutasaidia kupunguza changamoto za upatikanaji wa maji ambapo kwa sasa wakazi wa mji huo wanapata maji kwa mgao kila baada ya siku tatu na kueleza mipango ya ujenzi wa mradi mkubwa wa maji kutoka mito ya safu za milima kipengere.

Kwa upande wake mkurugenzi wa mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira  mji wa  Iringa IRUWASA Gilbert Kayange ameitaja miradi ambayo bodi ya mamlaka hiyo inaisimamia kwa mikoa ya njombe na Iringa na kuwa iko katua hatua za mwisho kukamilika.

 

Post a Comment

0 Comments