TANGAZA NASI

header ads

Wizara ya maji yaokoa zaidi ya Bil 5 zilizotarajiwa kupelekwa kwenye mradi wilayani Makete

 


Na Amiri Kilagalila,Njombe

Wizara ya maji na umwagiliaji nchini Tanzania imeokoa zaidi ya bil 5 zilizokuwa hatarini kutafunwa katika mradi wa maji kata ya Kinyika Tarafa  ya Matamba wilayani Makete  mkoani Njombe ambao umefikia asilimia 98 na kughalimu shilingi milioni 900 huku mpaka kukamilika kwake ukitarajia kugahalimu Bil 1.5 badala ya bil 6.7 zilizokuwa zimepangwa awali kutumika.


Mafanikio hayo yamebainishwa na Naibu waziri wa maji Jumaa Aweso wakati wa ziara yake ya kikazi mkoani Njombe ambapo amesema serikali imekuwa ikipoteza fedha nyingi katika miradi inayotekelezwa na wakandarasi na kuagiza mamlaka za maji kuanza kutumia
Force Account na wataalamu wa serikali katika kutekeleza miradi hiyo.

“Mradi huu ulitaka kutekelezwa kwa Bil 6.7 sisi baada ya kufanya ziara tukasema hapana,msituambie tu Bil.6.7 mkatuuzia mbuzi kwenye gunia,kwasababu wizara ya maji imeajili wataalamu,tunakabidhi kazi hii kwa wataalamu wetu badala ya kumpa mkandarasi na mradi mpaka sasa upo 98% wametumia milioni 900”Alisema Aweso


Aidha kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Njombe Ruth Msafiri amemueleza naibu waziri kuwa licha ya wizara kuendelea kupambana na swala la maji lakini bado kuna vijiji na miji inakumbwa na uhaba wa huduma ya maji.


“Hapa kuna changamot kubwa sana ya maji lakini ukizungumza na mamlaka anakwambia mpaka aende Iringa na sisi kasi ya mji inakuwa tunaomba sana tusaidiwe na kwamba mradi wa Hagafilo ukikamilika tutapata maji nay a ziada”alisema Ruth Msafiri

 

Naye kaimu meneja wa RUWASA wilaya ya Makete Injinia Innocent Lyamuya,amesema mradi huo utakapokamilika utawafikia jumla ya wakazi 15,320 wa vijiji 9 vya tarafa ya Matamba.

 

“Mradi huu ukikamilika utahudumia vijiji vipatavyo tisa vya Matamba,Kinyika,Mpangala,Ngonde,Mboje,Mbela,Mlondwe,Nungu pamoja na Ndapo.Eneo la mradi huu lina jumla ya wakazi wapato 15,320 ambapo mpaka sasa wanaopata huduma ya maji safi ni wakazi 13821 sawa na asilimia 90.2”alisema Lyamuya


Baadhi ya wananchi wa kata ya Kinyika akiwemo Zedekia Mahali wanasema awali kata hiyo lkuwa ikikubwa na changamoto kubwa ya ukosefu wa maji lakini kukamilika kwa mradi huo kumeongeza furaha kwao.

 

“Tunarudisha shukrani kwa niaba ya wananchi wote wa kata ya Kinyika,maji tunayo ya kutosha na nyumbani wananchi wana amani”alisema Zedekia Mahali

Post a Comment

0 Comments