TANGAZA NASI

header ads

Njombe:Utaratibu mpya kwa wanufaika wa TASAF waanza na changamoto




Na Amiri Kilagalila,Njombe

Zoezi la uhakiki wa kaya zinazonufaika na mpango wa maendeleo ya jamii TASAF  limeanza kufanyika mkoani Njombe na walengwa wakikiri mradi huo kuwa msaada mkubwa kwao.

Katika halmashauri ya wilaya ya Njombe zoezi hilo limeanza katika kata na vijiji mbalimbali ambapo wakazi wa kijiji cha Ikuna baadhi ya walengwa hao  akiwemo John Kipapi na Sesilia Wudumbe wamesema fedha ambazo wamekuwa wakizipata zimekuwa zikiwasaidia katika kukidhi mahitaji mbalimbali ikiwemo kusomesha watoto,kufuga na hata kujenga licha ya kuiomba serikali iwaongezee kiwango cha fedha kama inawezekana.

“Mradi huu kwa kweli ni mzuri lakini kwa kuwa wengine ni fukara wakubwa basi ingeongezwa kidogo mpaka hamsini elfu ingesaidia sana,nah ii inasaidia kununua mbolea hata shughuli nyingine ndogo ndoo”alisema John Kipapi

Kenan Ngimbudzi ni mjumbe wa serikali ya kijiji cha Ikuna ambaye anatoa ushauri kwa serikali juu ya mabadiliko ya mfumo wa upokeaji fedha hizo ambazo kwa sasa zitaanza kutolewa njia ya benki au simu tofauti na hapo awali.

“Swala zima ni kuwaambia wanaowahudumia walengwa wasifanye hujuma,lakini kwa njia ya simu ukiangalila zoezi litarudi lile la makato na tutarudi kulele wakati fedha yenyewe bado ni ndogo,kwa hiyo swala la kuibiwa kwa walengwa naona litakuwa kama awali ambavyo wasaidizi  wa kaya walikuwa labda wanakabidhiwa”alisema Kenan Ngimbudzi

Kwa upande wake mwezeshaji wa TASAF  ngazi ya halmashauri bwana Godfrey Kitulama ameeleza namna zoezi lilivyokwenda na kwamba kumekuwapo na baadhi ya changamoto zikiwemo za baadhi ya wazee kusahau nyaraka muhimu kama vitambulisho vya nida na mpiga kura hatua ambayo imekuwa ikichelewa zoezi la kuhakiki.

“Zoezi linaendelea isipokuwa changamoto kubwa ni wanufaika wa TASAF  wengine hawana vitambulisho vya NIDA na wengine vya wapiga Kura lakini wenye navyo tunaweza kuwasajili na ambao hawana wamendelea kutafuta viambata hivyo na kinachosababisha walio wengi ni wazee ndio maana uelewa uko tofauti na wanakuja bila vitambulisho”alisema Godfrey Kitulama

Mradi wa TASAF  katika kipindi hiki cha pili awamu ya tatu umeanza kwa kufanya uhakiki wa walengwa sahihi ili kuwaondoa watu hewa wanaonufaika kinyume cha taratibu.



Post a Comment

0 Comments