TANGAZA NASI

header ads

Halmashauri yadhamiria Dodoma kuwa ya kijani



Na Jackline Kuwanda, DODOMA
Halmashauri ya jiji la Dodoma imesema kuwa itahakikisha kuwa Dodoma inakuwa ya kijani huku ikipiga marufuku ukataji wa miti na atakayetaka kukata miti kwa sababu yeyote ile ni lazima apate kibali kutoka kwa Ofisi ya mkurugenzi wa Jiji.
Halmashauri pia imetoa wito kwa wale wote waliopanda miti kuhakikisha wanaitunza vizuri miti hiyo.
Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa Idara ya mazingira na udhibiti wa taka ngumu katika halmashauri ya jiji la Dodoma bwana Dickson Kmaro wakati akizungumza na Mtandao wa Dodoma News Blog.
Amesema moja ya majukumu waliyonayo pamoja na majukumu mengine ya udhibiti wa taka ngumu ,upendezeshaji miji, wanajukumu jingine la uhifadhi na utunzaji wa mazingira  kwani katika eneo hilo jukumu ambalo wanaendelea nalo kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ni suala zima la kukijanisha Dodoma ambayo ni kampeni iliyozinduliwa na Makamu wa Rais Mh Samiah Hassan kaitka eneo la mzakwe. 
Dkt Liberatus Domic Lyimo ambaye ni mhadhiri mwandamizi wa chuo kikuu cha Dodoma UDOM amesema tangu walipoletewa miti walianzisha kampeni ya upandaji miti na vilevile wanaklabu za wanafunzi za mazingira . 
Mrakibu wa gereza  la Msalato Hamisi Nyaku amesema suala la kutunza mazingira katika Gereza lao wamelipa kipaumbele kwa kiasi kikubwa .
Halmashauri ya Jiji la Dodoma ipo makinikatika kutekeleza mikakati mbalimai ya kitaifa ya utunzaji na uhifadhi wa mazingira ikiwemo mkakati wa kuhifadhi ardhi na vyanzo vya maji
Viongozi wa ngazi mbalimbali wamekuwa msitari wa mbele katika kuhamasisha utekelezaji wa zoezi hilo akiwemo Mhe. Makamu wa Rais Mama Samia Hassan Suluhu aliyezindua kampeni ya kuifanya Dodoma kuwa ya kijani mnamo tarehe 21/12/2017 ambapo ilipandwa jumla ya miti 2,300 katika chanzo cha maji Mzakwe ambayo ilitolewa na TFS.



Post a Comment

0 Comments