TANGAZA NASI

header ads

Njombe:Kijana mbaroni kwa tuhuma za kumlawiti mwenzake wa miaka 15 akidai ni mpenzi wake



Na Clief Mlelwa,Makambako

Peter paulo Chaula (30) mkazi wa mtaa wa Kivavi mjini Makambako  mkoani Njombe anashikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za kumlawiti mwenzake mwenye umri wa miaka 15 akionekana kuwa na mazoea kutokana na madai kuwa ni mpenzi wake.

Akizungumza na kituo hiki kwa njia ya simu kamanda Issa amesema mtuhumiwa huyo anashikiliwa na jeshi hilo baada ya kupata taarifa hizo kutoka kwa wananchi.

“Kijana huyu Peter Chaula ni mfanyabiashara,ni hali isiyoyakawaida kwasababu baada ya kuwahoji wawili hawa inaonekana kuna mazoea ya hawa kufanyiana vitendo hivyo hivyo,kwasababu huyu mtoto wa kiume aliyekuwa anamlawiti mwenzake anasema ni mpenzi wake”alisema Hamis Issa

“Niwaambie watu wa Njombe wawe makini sana na vijana wa kiume kwasababu sasa hivi wameanza kufanya kama ushoga vile kwa hiyo hii ni hatari  huyu kijana wa kiume ni kijana ambaye anakaa kwa mamaake mkubwa na wazazi wake hawapo lakini vitendo hivyo vinatokea na watu walifanya mchezo na wakamkamata”aliongeza kamanda Issa

Aidha kamanda ISSA amesema  hali ngumu ya kiuchumi ni miongoni mwa sababu zinazopelekea watu wengi kujihusisha na vitendo hivyo na amewaka wananchi kuendelea kutoa taarifa za watu wanaojihusisha na matukio ya kiuharifu.
June 18 mwezi huu wananchi wa mtaa wa kivavi mjini makambako waliitaka serikali kuwachukulia hatua za kisheria  watu wote wanaojihusisha na matukio hayo ya ulawili.

“Tulivyofika kwenye ile nyumba ambayo mtuhumiwa alikuwepo na Yule kijana tukajaribu kusikiliza dirishani tukakauta kweli kuna watu wanafanya mazingira ambayo sio ya kawaida,tukagonga mlango akaja kufungua Yule kijana na Yule mtuhumiwa alikuwa amekaa kitandani amevua tisheti na koti lilikuwa pembeni.Na mimi hapa alishawahi nifuata aliniambia anahitaji kulala na mimi”walisema wananchi wawiti tofauti.


Post a Comment

0 Comments