TANGAZA NASI

header ads

Muandaji muziki mkongwe maarufu kwa jina la Master J atangaza nia ya kugombea ubunge jimbo la Rombo



Joachim Marunda Kimaryo (maarufu kama Master J  ni muandaaji wa muziki nchini Tanzania amesema

“Mimi nina miaka 50 kasoro miaka 3, nimefanya mengi, Kiwanda cha Muziki kimenipa mengi, Watoto wangu wanasoma chuo Nje ya nchi wa kwanza na wapili, hivyo mafanikio nimeshapata, ni muda sasa kwenda kuwatumikia Raia wa Rombo kwa kuwa Mbunge wao”-
(via XXL ya Clouds FM)

“Sijawahi kuisaidia jamii yangu ya Watu wa Rombo, Mungu amenijaalia uwezo kiasi hivyo nafahamu matatizo yanayoikumba Rombo na ningependa kuwasaidia, hivyo hilo ndio jambo linalonisukuma zaidi”-
(via XXL ya Clouds FM)

"Mimi nipo CCM tangu zamani, natangaza nia, uchaguzi wa mwaka huu, Chama kikinipa nafasi nitagombea Rombo, Kilimanjaro kule ndio kwetu, Mbunge wa sasa kule ni Mzee wetu Selasini, naenda Rombo ili kuwatumikia Wananchi” -
(via XXL ya Clouds FM)

“Kuhusu kufunga ndoa na Shaa tumekamilisha mipango, mwaka huu lolote linaweza kutokea, kwa kuwa nimetangaza nia ya kugombea Ubunge kule Rombo, Kilimanjaro mwaka huu, najua ukiingia kwenye siasa moja ya silaha wataitumia ni hiyo hajaoa anaishi na hawara”-
(via XXL)

Post a Comment

0 Comments