TANGAZA NASI

header ads

Jamii yaendelea kuhamasishwa kuona umuhimu wa kufanya ufuatiliaji wa miradi na huduma zinazotolewa




DODOMA 

Shirila la Raleigh Tanzania linaendelea  na Kampeni yake ya Uwajibikaji wa Jamii Kupitia Vijana yenye lengo la kuhamasisha jamii nyingi kuona umuhimu wa kufanya ufuatiliaji wa miradi na huduma zinazotolewa.

Mradi huo unatumia Mfumo wa kujenga jamii adilifu ambao unashirikisha wananchi wenyewe kutafuta suluhisho la changamoto zinazojitokeza kwenye miradi au  huduma katika jamii.

Akizungumza kwa njia ya simu na kituo hiki kuhusiana na jamii yenye uadilifu, Mratibu wa kampeni hiyo kutoka wilayani Chamwino William Luhunde amesema kuwa jamii yenye uadilifu ni mfumo ambao umewekwa kwaajili ya kuongeza uwajibikaji na uwazi katika utekelezaji wa miradi.

‘’Lakini katika mfumo huu ni mfumo unao wezesha makundi maalumu kama wanawake ,vijana na watu wanaoishi na ulemavu lengo kuu ni kuwafanya washiriki katika kutoa maoni yao kuhusu miradi’’ Wiliam

Kuruthumu Ayubu yeye ni mfuatiliaji wa miradi ya jamii katika kampeni hiyo kutoka wilayani chemba kijiji cha Mtoro Mkoani hapa amesema kuwa wanakijiji wa kijiji hicho wamekuwa wakiwajibika ipasavyo kwani mradi huo wameweza kuupokea vizuri .

‘’Wameupokea mradi huu vizuri wanautunza hawauharibu na wanajua kabisa unafaida ndio maana wanatunza na wawajibika kuutunza sio mmoja ni wote wanaume,wanawake,watoto hasa vijana’’Kuluthumu 

Akizungumzia maendeleo ya vijana katika mradi na nini kifanyike, Mratibu wa kampeni Dodoma Mjini Halima Seleman amesema kuwa vijana wanamchango mkubwa wa kuhakikisha kuwa miradi waliyonayo inakuwa na mafuaa katika jamii .

‘’kuna vijana ambao ni wafuatiliaji wako katika vijiji na mitaa mbalimbali ambayo tunafanya kazi au tunatekeleza mradi huu ,kwanza kabisa vijana tunatakiwa kupewa elimu ya umuhimu wa sisi kushiriki katika miradi mbalimbali ya maendeleo tupewa kipaumbele pale yanapokuja masuala ya kimaendeleo katika jamii yetu kwasababu tunaamini kwamba vijana ndio nguvu kazi ya Taifa’’ Halima 

Lengo la kampeni hiyo ni Kuhamasisha jamii kufanya ufuatiliaji wa miradi na huduma katika maeneo yao na kuwa wawajibikaji lakini pia Kuhamasisha wananchi kupata taarifa kuhusu miradi na umuhimu wa kushiriki kwenye pamoja na Kufahamu umuhimu wa Uwajibikaji katika jamii na kuunda Kikundi kazi ili kutatua changamoto.

Raleigh Tanzania ni shirika lisilo la kiserikali linalofanya kazi katika kusaidia miradi ya maendeleo endelevu na imejikita katika kufanya kazi kwa kushirikiana na vijana kwa kuwahamasisha kuleta maendeleo chanja katika maeneo makuu ambayo ni kujenga jamii isiyo tegemezi (Community Resilience),Maji na usafi wa mazingira (water anda sanitation na kuwawezesha vijana katika ujuzi na uwezo wa uongozi (Youth Leadership)




Post a Comment

0 Comments