TANGAZA NASI

header ads

Idara ya Vyuo na Vyuo Vikuu {Uvccm} Njombe yatema cheche.



Na Zakayo Chelesi

Idara ya vyuo na vyuo vikuu Uvccm Mkoa wa Njombe imejitokeza kumdhamini mwenyekiti wa Ccm taifa ambaye pia ndiye Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt John Pombe Magufuli  huku ikieleza kuwa wamejipanga kuleta ushindi wa kishindo katika uchaguzi mkuu kwa mwaka 2020-2025.


Akizungumza Mwenyekiti wa Idara hiyo Seleman Matembwi amesema kuwa wao kama vijana wa vyuo ndani ya umoja wa vijana Uvccm mkoa wa Njombe wameamua kumdhamini Rais Magufuli  kwa sababu ya juhudi zake alizo zioenyesha katika kipindi cha miaka mitano kwa mafanikio makubwa aliyoyafanya  nchini Tanzania.


Sambamba na hayo Mjumbe wa idara hiyo mkoa wa Njombe  Chrispin Kalinga ameongeza kwa kusema kuwa wao kama vijana wa mkoa wa Njombe wamejipanga vizuri kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2020-2025 kuhakikisha wanakipatia ushindi wa kishindo wa chama cha mapinduzi Ccm katika ngazi za madiwani,Wabunge na Rais.


Mjumbe huyo aliongeza kwa kuwataka vijana wa mkoa wa njombe kuhakikisha wamejipanga kikamilifu kuona namna wanavyo weza kukisaidia chama kupata ushindi katika uchaguzi mkuu kwenye maeneo yao.


Katika hatua nyingine Mwakalinga akaongeza kwa kuwaomba vijana wajitokeze kuwanania nafasi mbalimbali za uongozi ikiwemo udiwani na ubunge kwenye maeneo yanayo wazunguka akiamini vijana wanaweza.


“Naomba nitumie nafasi hii kuwaomba vijana wenzangu msisite kujitokeza pindi taarifa za kuanza kujaza fomu mkoani kwetu itakapo tangazwa rasmi mjitokeze mkachukue na kujaza nafasi mbalimbali haswa ya Udiwani na ubunge naamini vijana ni nguvu kazi ya taifa na tunaweza kikubwa ni ku jiamini na kudhubutu kwasababu sisi ni nguvu kazi ya leo na ni chachu ya  maendeleo ya Njombe na taifa kwa ujumla.”aliyasema Mwakalinga.


Pia baadhi ya wanafunzi kutoka vyuo mbalimbali ikiwemo chuo cha Amani na chuo cha Ekros sabasaba walio jitokeza kumdhamini Rais Magufuli wamongea kwa kusema kuwa wao hawajalazimshwa na mtu bali ni kwa hiyali yao kumdhamini kiongozi huyo kwasababu ya mambo makubwa aliyo yafanya katika msimu unao isha.


Wakamaliza kwa kusema kuwa wao kama wanafunzi wa idara ya vyuo na vyuo vikuu Ccm wamejipanga kikamilifu kuhakikisha wanafanya mageuzi katika mkoa wa njombe kwa kuhakikisha kila kata za mkoa wa Njombe pamoja na majimbo yote yaliyomo kwenye mkoa huo chama cha mapinduzi kinatawala.



Post a Comment

0 Comments