TANGAZA NASI

header ads

Waziri Jafo aagiza madaktari wapya,kufika vituo vyao vya kazi ndani ya wiki mbili


 

Na Jackline Kuwanda,Dodoma

Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais,Tawala za mikoa na Serikali za mitaa (TAMISEMI) Seleman Jafo amewataka madaktari wapya 610 walioajiriwa  chini ya mamlaka za mitaa hivi karibuni kuhakikisha ndani ya wiki mbili kuanzia mei 11 mwaka huu  wanaripoti katika maeneo waliyopangiwa.

Kuajiriwa kwa madaktari hao kunafanya idadi ya madaktari walioajiriwa tangu serikali ya awamu ya tano iingie madarakani chini ya Rais Dkt John Magufuli kufikia 9,839 katika mamlaka za serikali za mitaa.

Akizungumza na waandishi wa habari leo ofisini kwake jijini Dodoma Jafo amesema madaktari hao wamepangiwa katika vituo vya Afya,Zahanati na Hospitali za wilaya.

Ametoa maagizo kwa madaktari hao ikiwemo kwenda kuongeza weledi kwenye maeneo yao katika kupambana na virusi vinavyosababisha ugonjwa wa homa kali ya mapafu(COVID 19) na pia kuhakikisha wanaripoti wakiwa na vyeti vyao vya taaluma.
  
Februari 20 Rais Magufuli akifungua mkutano wa 55 wa Chama Cha Madaktari Tanzania(MAT)na watumishi wa sekta ya afya uliofanyika katikaukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Julius Nyerere(JNICC)alitangaza kuajiri madaktari 1,000.

Mwezi mmoja baadae TAMISEMI ilitangaza ajira hizo 610 na kuwataka waombaji waombe kuanzia Machi 24 hadi April 10 ambapo zoezi hilo lilifungwa.

Post a Comment

0 Comments