TANGAZA NASI

header ads

Sheria ya usalama barabarani 1973 Mbioni kurekebishwa ili kuendana na mahitaji ya sasa.






Na Jackline kuwanda, DODOMA

Ajali za Barabarani zimetajwa kuwa kama sababu namba moja ya vifo kwa watoto wa umri kati ya miaka 5 hadi 14 pamoja na vijana wa umri kati miaka 15 hadi 29 ambao ndio nguvu kazi ya Taifa.

Takwimu zinaonesha kuwa bado idadi ya vifo na majeruhi ni kubwa licha ya juhudi zinazofanyika kwani ajali hizo zimekuwa zikiigharimu serikali kurekebisha miundombinu,kufanya maokozi,kupoteza nguvu kazi ya Taifa na vifaa tiba Hospitalini.

Akifungua kongamano la Usalama wa Barabarani jijini Dodoma ikiwa ni Muungano wa Asasi za Kiraia zinazo shawishi Maboresho ya sheria ya usalama Barabarani,Waziri wa mambo ya ndani ya Nchi Mh George Simbachawene amesema kuwa wanachi wengi wamekuwa wakipoteza wapendwa wao katika ajali na baadhi kusababishiwa ulemavu na majereha ya kudumu hivyo kupitia wizara yake amesema ipo katika mchakato wa kurekebisha sheria ya usalama barabarani 1973 ili iweze kuendana na mahitaji ya sasa.

Amesema kama serikali wanayo nia ya dhabiti ya kuhakikisha kwamba ajali zinapungua kwa asilimia 50% ifikapo 2030 kama ambavyo wameahidi katika mikataba ya kimataifa na kama matakwa ya sheria za kimataifa zinavyosema huku akitoa wito kwa madereva wanao endesha magari kuzingatia sheria za barabarani kwani wako madereva wanao endesha kwa mwendokasi ,wakiwa wamelewa na ameliagiza jeshi la usalama barabarani kuchukua hatua kali dhidi ya wale wote wanaokiuka sheria za usalama Barabarani.

Akizungumzia masuala ambayo mtandao unafanyia uchechemuzi Rose Reuben ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa TAMWA  amesema kuwa  mtandao unafanya uchechemuzi juu ya mfumo bora wa kisheria juu usalama wa barabarani ili kuhakikisha kuwa ajali za Barabarani zinapungua ikiwa ni pamoja na majeraha yatokanayo na ajali barabarani pamoja na vifo.

Amesema mtandao ulianzishwa kwa malengo kadhaa ikiwa ni pamoja na kuwa na sauti ya pamoja katika kuendesha kampeni ya kushawishi maboresho ya sheria ya usalama barabarani .

Hatahivyo, Takwimu za Shirika la Afya ulimwenguni zinaonesha kuwa zaidi watu 1,350,000 hufariki kwa ajali za barabarani duniani kote.


Post a Comment

0 Comments