TANGAZA NASI

header ads

Polisi Dodoma wanasa magari 17 yanayosadikika ya wizi




DODOMA

 Jeshi la Polisi mkoani Dodoma limekamata magari 17 yanayosadikiwa ya wizi katika maeneo tofauti ya mkoa wa Dodoma yakiwa yamebadilishwa pleti namba pamoja na namba nyingine kwenye vioo.

Kamanda wa polisi mkoani Dodoma Gilles Muroto leo amewaambia waandishi wa habari kuwa magari hayo yamekamatwa katika msako ulioanza Mei 19 hadi 22, 2020 yakiwa na makosa tofauti ambayo yaliwafanya kutambua kuwa magari hayo yanasadikiwa kuwa ya wizi. 

Muroto amesema magari hayo yamekutwa baada ya kubainika yanatumia cadi na file za magari mengine yaliyopata ajali, yaliyokatwa chassis na kuunganishwa kwenye magari mengine, namba za chassis kuingiliana na magari mengine, kufuta baadhi ya namba au kuongeza au kubadilisha au kubandika vibati vya magari mengine.

Mbali ma matukio hayo na magari jeshi la polisi linamshikilia Festo Lalika akiwa na vifaa vya pikipiki, jenereta mbili na injini moja ya bajaji huku Lello Ringo akimatwa na TV tatu, vifaa vya kuvunjia pamoja na panga ambapo hapa kamanda Muroto anaeleza zaidi.

Hata hivyo amesema ili kuifanya makoa makuu kuwa salama jeshi la polisi mkoani Dodoma kwa kushirikiana na mikoa jirani watafanya kazi kwa pamoja ili kuwadhibiti wahalifu.


Post a Comment

0 Comments