TANGAZA NASI

header ads

Wananchi wawajia juu wenzao kwa kuuza eneo la kijiji lililotengwa kwa ajili ya Kilimo na Ufugaji




Na Amiri kilagalila,Njombe

Wananchi wa vijiji vya kata ya Itulahumba halmashauri ya wilaya ya Wangingombe mkoani Njombe kwa pamoja wamepinga kitendo kinachofanywa na baadhi ya wananchi wenzao kwa kushirikiana na mtendaji wa kijiji hicho kuuza eneo ambalo limetengwa kijijini hapo kwaajili ya ufugaji na kilimo. 
                                                                      
Eneo hilo lenye ukubwa wa zaidi ekari 80 ambalo limeanza kukatwa miti na kulimwa bila makubaliano ya kamati za vijiji pamoja na mkutano wa hadhara wa wananchi Hao Akiwemo Yohana Mgute na Mary Mwakajuba wamesema serikali isaidie waliovamia kukamatwa na kuzuia uharibifu unaoendelea.

“Eneo hili lirudi serikalini bila kujali kuna watu wamepata visenti kwa kuuza sisi tunataka eneo lirudi”alisema Yohana Mgute
Mtendaji wa kijiji hicho Rudlof Mbilo anasema eneo hilo licha ya kuwa limetengwa kwajili ya shughuli za kilimo na ufugaji lakini  hakuna nyaraka zinazothibitisha na ndio sababu amekuwa akiidhinisha watu kuuziana ardhi hiyo.

“Hizo ekari tano zilizoanzwa kuuzwa alionwa mwenyekiti wa kijiji pamoja na mimi huku mmuzaji akihitaji kuuza ekari kumi”alisema Rudlof Mbilo

Viongozi wa kata hiyo wakiongozwa na diwani Thobias Mkane na Betty Mangula Afisa Mtendaji wa Kata Hiyo wamepiga marufuku   mtu yeyote kufanya shughuli katika eneo hilo wakati uchunguzi wa kuwabaini waliovamia na kuuza ukiendelea.

“Sasa tunasimamisha eneo lile lisiendelee kutumika tena,sisi tunayefahamu hapa tumepokea madaraka mpaka mara tatu lakini hatujaona mtu akiishi mle,kwa hiyo liachwe kutumika mpaka ufumbuzi utakapopatikana”Alisema Thobias Mkane
                                                                                                               

Post a Comment

0 Comments