TANGAZA NASI

header ads

Dodoma:Waandishi wa habari waishukuru TAMWA



Na Jackline Kuwanda,DODOMA

Waandishi wa habari Jijini Dodoma wamekishukuru Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake (TAMWA) kwa kuwapatia mafunzo ya usalama wa kimtandao (Cyber Security Training) kwani imekuwa ni njia moja wapo ya wao kufahamu matumizi sahihi ya mtandao. 

Wakizungumza mara baada ya kumalizika kwa mafunzo hayo waandishi hao akiwemo Veronika komba pamoja na Ronald Sonyo wamesema kuwa kupitia mafunzo hayo wamejifunza mengi kikubwa watazingatia yale yote waliyofundishwa na wao kwenda kuwafundisha wengine kuhusiana na matumizi mazuri ya mtandao hasa wakiwa kama wanahabari.

Godwin Assenga ambaye ni mratibu wa mradi wa usalama wa kimtandao (Cyber Security Training )kutoka TAMWA ambaye ndiye alikuwa akitoa mafunzo kwa waandishi wa habari amesema kuwa mradi huo wameundaa kwa wanahabari ambao wamekuwa wakifanya nao kazi kwa ukaribu baada ya kuona kuna ulazima wa kuhakikisha usalama kwa wanahabari katika mitandao huku akieleza lengo la mafunzo hayo.

Akifunga Mafunzo hayo mkurugenzi mtendaji wa TAMWA Bi Rose Reuben amewataka wanahabari ambao wamepata mafunzo hayo kwenda kuyafanyia kazi katika maeneo yao.

Hatahivyo,wanahabari wameendelea kusisitizwa kuzingatia matumizi sahihi ya mtandaoni ili matatizo mengine yasiweze kujitokeza kwani watu wengi wamekuwa wakifuatilia mitandao hivyo kama mwandishi ataenda kinyume na matumizi mazuri ya mtandao basi anaweza kukumbana na matatizo.

Post a Comment

0 Comments