TANGAZA NASI

header ads

Marekani yatangaza vikwanzo dhidi ya viongozi wa Mapinduzi Myanmar



 Rais wa Marekani Joe Biden ameidhinisha agizo la watendaji kuweka vikwazo kwa viongozi wa mapinduzi ya Myanmar.

Hatua hizo zimechuliwa dhidi ya viongozi wa jeshi, familia zao na wafanyabiashara wanaohusishwa nao.

Hatua pia zinachukuliwa kuzuia jeshi kuzipata fedha kiasi cha dola bilioni 1 pesa za serikali zinazoshikiliwa Marekani.

Vikwazo hivyo vinakuja wakati ambao mwanamke aliyepigwa risasi kichwani wakati wa maandamano akipigania maisha yake hospitalini katika mji mkuu wa Nay Pyi Taw.

Mya Thwe Thwe Khaing alijeruhiwa Jumanne wakati polisi walipojaribu kuwatawanya waandamanaji kwa kutumia maji, risasi za mpira na risasi za moto.

Maelfu wamejitokeza katika maandamano ya barabarani kupinga mapinduzi ya wiki iliyopita, ambayo yalipindua serikali ya Aung San Suu Kyi iliyochaguliwa kidemokrasia licha ya marufuku ya hivi karibuni ya mikusanyiko mikubwa na amri ya kutotoka nje usiku.

Kumekuwa na ripoti za majeraha mengine mabaya kwani polisi wameongeza matumizi ya nguvu, lakini hakuna vifo hadi sasa.

Post a Comment

0 Comments