TANGAZA NASI

header ads

Njombe:Wachangamkia msimu wa matunda (Makusu)



Na Amiri Kilagalila,Njombe

Wakati matunda pori na mizizi yakitumika kama chakula  katika zama za mawe za kale,kwa zama za sasa za chuma yameonekana kuwa matunda bora na ya kibiashara yanayowaingizia watu kipato cha kila siku.

Utajiri wa matunda pori mkoani Njombe unawapa  fursa wenyeji wa mkoa huo kuyatumia  kuboresha lishe pamoja na kibiashara. 

Hata hivyo Mkoa wa Njombe umebarikiwa kuwa na matunda ya aina mbalimbali yakupandwa pamoja na matunda pori  ambayo  hustawi katika maeneo mengi ya porini.

Matunda  yamekuwa yakiwapa fursa ya kibiashara  wenyeji kama ilivyo kwa  Theresia Mwajombe  ambaye kila unapofika msimu wa matunda pori huchangamkia fursa kwa kwenda porini na kukusanya matunda  kwa ajili ya biashara.

Kwa sasa ni msimu wa matunda pori wenyewe wanayaita masaulwa  pamoja na makusu.

"Nikiokota huku porini naenda nyumbani nachukua mkeka,nayaanika harafu asubuhi nayaweka kwenye kapu harafu nayafunga na kuyapeleka mjini"alisema Theresia Mwajombe  

Anachokifanya Theresia baada ya kukusanya matunda  porini akiwa na kijana wake James Emilio ni kuyafungasha na kuyahifadhi vizuri na kisha kuyaagiza mjini kupitia  vyombo vya usafirishaji ambako huwasiliana na wafanyabiashara wenzake ambao wanapokea na kuwajumlishia wafanyabiashara wengine Ikiwa kwa siku moja huokota zaidi ya debe tano na kila debe moja huuza kwa shillingi elfu mbili.

"Tukishayaokota huku porini tunayapeleka nyumbani na kuyahifadhi kwenye kihifadhio kizuri ili yafike mjini bila kupasuka pasuka"

Sabrina kapinga ni miongoni mwa wanaopokea matunda kutoka vijijini , akishayapokea huwauzia wanaojumua kwa ajili ya kwenda kuuza kwa rejareja kwenye vipimo vidogo.

"Kuna mtu anayenitaftia kule kijijini harafu namwambia apime debe na kwa mimi nachukua kuanzia debe tano na wateja ni wengi na akina wafanyabiashara ni wengi pia wanajishughulisha sana"alisema Sabrina kapinga 

Wafanyabiashara hawa wanasema hawapati fedha nyingi lakini inayopatikana inawasaidia kujikimu Kimaisha Huku Walaji na watumiaji akiwemo Steward Mngalilwa wanaeleza namna wanavyofurahia kula matunda pori.

"Kuna watu wengine wanayaokota kule mdandu yanayodondoka chini na wanayaagiza kwenye gari,sahizi ndio msimu wenyewe,haya matunda hayana chemical yanasaidia kinga mwilini ndio maana wanyama wa porini wanaishi kwa ajili ya kula matunda haya"alisema Steward Mngalilwa 

Pamoja na matunda pori wapo pia wanaojihusisha na shughuli nyingine za porini ikiwemo utegaji wa mizinga ya nyuki  kwa ajili ya kujipatia asali.

Post a Comment

0 Comments